PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: JKT OLJORO, AFC KUWEKA WAZI MAJEMBE YAO.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Na; YOHANA CHALLE. PrincemediaTZ Timu ya maafande wa Jkt Oljoro inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara inatarajia kuc...

Na; YOHANA CHALLE. PrincemediaTZ


Timu ya maafande wa Jkt Oljoro inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania bara inatarajia kuchuana vikali na ndugu zao AFC katika ufunguzi wa ligi maalum ya Nyerere Cup inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi septemba 10 jiji hapa.

Tayari timu ya zote zimethibitisha kushiriki michuano hiyo huku kila mmoja akijitamba kuonyesha ubabe dhidi ya mwenzake na pia wakitumia mechi hiyo kutambulisha wachezaji waliosajiliwa kwa wapenzi wa Soka wa jiji Arusha.

Mechi hiyo ya ufunguzi kati ya Oljoro na AFC itakayochezwa  katika uwanja wa Sheik Amri Abeid, ni kwa ajili ya kufungua michuano ya Nyerere Cup itakayoshirikisha Jumla ya timu Sita za vijana chini ya umri wa miaka 13, lengo kubwa ikiwa ni kumuenzi muasisi wa Taifa hili Hayati Mwl, Julius K. Nyerere.

Akizitaja timu shiriki katika mashindano hayo, mratibu wa maadhimisho hayo Bertha Ismail alisema kuwa ni pamoja na Nyota Accademy, Future Star, Kijenge Youth zingine ni Rolling stone, Young Life na Pallot.

“Maadhimisho hayo huwa yanafanyika kila Octoba 14 kila mwaka lakini kwa mwaka huu tunafanya mwezi Septemba ili maadhimisho haya yasiathiriwe na zoezi la Uchaguzi ambapo pamoja na kumuezi Muasisi wa Taifa letu lakini mashindano haya pia inalenga kuhamasisha wananchi wafanye uchaguzi kwa amani bila vurugu ili sekta ya utalii hapa nchini izidi kukua” alisema Ismail

maadhimisho haya yatafunguliwa na mkurugezi wa jiji la Arusha Iddi Juma “kauli mbiu ni Uchaguzi wa amani 2015: Taifa Moja kwa Maendeleo ya utalii” ambapo wadau mbali mbali wa maendeleo ya nchi yetu na utalii kwa ujumla watahudhuria ufunguzi na kilele ambayo ni septemba 19 na atakayefunga ni mkurugenzi wa hifadhi ya Taifa (TANAPA)  Allan Kijazi.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top