PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: HABARI PICHA MASHINDANO YA MPIRA WA WAVU TAIFA ILIYOFANYIKA SHEIKH AMRI ABEID STADIUM JIJINI ARUSHA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
mchezaji wa timu ya wavu ya Mkoa wa Tanga wanawake waliovaa jezi ya Bluu akipiga mpira katika mashindano ya wavu klabu bingwa Tanzania...

mchezaji wa timu ya wavu ya Mkoa wa Tanga wanawake waliovaa jezi ya Bluu akipiga mpira katika mashindano ya wavu klabu bingwa Tanzania katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha kati ya Dodoma wanawake na Tanga yaliyomalizika mwishoni mwa wiki, Tanga walishinda kwa seti 3-0. Picha na Yohana Challe

TIMU zaa JKT Mbweni kutoka Dar es salaam  kwa  wanaume na wanawake zimefanikiwa kuchukua ubingwa wa wavu Tanzania msimu wa 2015 baada ya kufanya vyema katika mashindano ya klabu bingwa wavu  yalilomalizika mwishoni mwa wiki jijini hapa.

Mashindano hayo yaliyoendeshwa kwa mtindo wa ligi yalimalizika kwa timu kwa wanaume timu ya Jkt Mbweni kunyakua ikiwa na jumla ya pointi 15,ikifuatiwa na timu ya Tanga ilijikusanyia jumla ya pointi 12,nafsi ya tatu iliwaendea timu ya Pentagone ya Arusha kwa pointi 9 ,huku Dodoma wakipata jumla ya pointi 6 ,Karatu pointi 3 na timu ya Flowers Arusha ikikosa pointi na kushika mkia.

Maafande hao wa JKT Mbweni pia kwa wanawake walimaliza mashindano hayo wakiwa na pointi 6 wakifuatiwa na Tanga kwa pointi 3  huku Dodoma nao wakimaliza bila pointi.

Michuano hiyo ya Klabu Bingwa wavu  Tanzania ilichezwa kwa siku tatu katika viwanja vya sheikh amri abeid pamoja na viwanja vya pentagon klabu, huku ikiwa chini ya chama cha wavu mkoa wa Arusha (AVA) Pamoja na chama cha wavu Tanzania (TAVA).

Akifunga mashindano hayo  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoaa wa Arusha, Mwanvita O. Okeng’o  ambaye ni afisa michezo mkoa aliwasihi wacheze mbalimbali kuongeza juhudi katika kuhakikisha wanahamasiha mchezo wa wavu unakuwa na wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu.

Naye Makamo mwenyekiti wa  chama cha wavu Tanzania (TAVA) Muharini Mchume alieleza kuwa pamoja na kuwa timu sita pekee ndizo zimechuana vikali zimeweza kuonyesha ushindani wa kipekee kwani zilionekana kuchuana vilivyo.
“Mashindano yamekwenda vizuri natunawashukuru chama cha wavu Arusha  (AVA) kwa maandalizi makubwa yaliyowezesha kufanyika kwa michuano hii vile vile shukrani kwa wazamini mbalimbali waliojitokeza kutuunga mkono” alisema Mchume

Aliongeza kuwa mwenyekiti wa chama cha wavu Tanzania (TAVA) Augostino Hagapa  hakuweza kufika kutokana na kuteuliwa kuwa ‘Match Commissioner” katika mashindano ya wavu ya  All Africa Games yanayotarajiwa kuanza mapema mwezi septemba nchini Congo,akimuwakilisha  Rais wa shirikisho la wavu Afrika.

Aidha chama cha wavu mkoa wa Arusha kimekabidhiwa mipira mitatu na chama cha wavu Tanzania (TAVA) vile vile kilimkabidhi mgeni rasmi mpira mmoja kwa ajili ya mazoezi.  

Mabingwa watetezi wa michuano hiyo ya wavu 2014  timu ya Magereza kwa wanawake kutoka jijini Dar es salaam pamoja na timu ya BOT ya jijini Mwanza kwa wanaume nazo pia hazikuweza kufika na kutetea ubingwa wao.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top