PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: RAISI KIKWETE AHIMIZA UJENZI WA BARABARA ZA VIJIJINI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Na Ferdinand Shayo,Arusha. Raisi Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa serikali za mitaa kuhakikisha kuwa wanajenga bara...


Na Ferdinand Shayo,Arusha.



Raisi Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa serikali za mitaa kuhakikisha kuwa wanajenga barabara maeneo ya vijijini ili kuchochea maendeleo katika  maeneo ya vijijini na kufungua fursa mbalimbali za kiuchumi zilizoko katika maeneo hayo.



Kikwete amesema hayo jana wakati akihutubia mkutano wa Viongozi wa serikali za mitaa (TAMISEMI) uliowakutanisha wakuu wa mikoa,wilaya,Pamoja na Wakurugenzi  kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa ubora wa kazi  na barabara endelevu,Raisi Kikwete amesema kuwa ujenzi wa barabara vijijini utafungua milango ya maendeleo vijijini na kubadilisha maisha ya watu wengi



Pia Rais Kikwete amewataka Viongozi wa Serikali za mitaa kuwa waaminifu katika kusimamia mfuko wa barabara ambao umefikia kiasi cha shilingi bilioni 800 ili mfuko huo uweze kuwahudumia Watanzania badala ya kuwanufaisha watu wachache.



“Fedha hizi za mfuko wa barabara zikitumika vizuri zitapunguza matatizo ya miundombinu ya barabara yanayozibili sehemu nyingi nchini” Alisema Kikwete





Waziri wa TAMISEMI ,Hawa Ghasia amesema kuwa wizara yake imeanzisha idara kamili ya Miundombinu ambayo itafanya ukaguzi na kuzuia hasara inayotokana na ujenzi wa barabara chini ya kiwango.

Ghasia alisema kuwa kumekua na changamoto ya fedha inayokwamisha ukarabati wa barabara za mitaa ambazo husiadia upanuzi wa miundombinu katika maeneo mbali mbali.





Katibu Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI ,Jumanne Safini  amesema kuwa Wizara hiyo inakabiliwa na changamoto ya  kukosekana kwa rasilimali za kutosha  hali inayosababisha viwango duni vya barabara vinavyotokana na kukosekana kwa usimamizi  na ukaguzi  hivyo kutopata barabara endelevu.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top