PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: SERIKALI IMETAKIWA KUWEKEZA KWENYE MASOMO YA SAYANSI ILI KUPANUA WIGO WA AJIRA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Na Ferdinand Shayo, PrincemediaTZ Serikali imetakiwa kuwekeza kwenye masomo ya sayansi ili kupata wataalamu wa kutosha ka...


Na Ferdinand Shayo, PrincemediaTZ

Serikali imetakiwa kuwekeza kwenye masomo ya sayansi ili kupata wataalamu wa kutosha katika Nyanja mbalimbali na kupanua wigo wa ajira ili kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla.

Wakizungumza katika Harambee ya ujenzi wa Maabara zilizoko wilaya ya Rorya mkoani Mara iliyofanywa na wenyeji wa wilaya hiyo jamii ya wajaluo na WanaMara waishio mji mdogo wa Mirerani wilaya Simanjiro Mkoa wa Manyara wamesema kuwa ujenzi wa maabara utasaidia kuchochea maendeleo kupitia sayansi.

Raphael Alex Ombade ambaye ni Katibu wa kuwezesha ujenzi wa Maabara wilaya ya Rorya  amesema kuwa ili nchi iweze kuhimili ushindani wa kimataifa na soko la dunia kwa ujumla hawana budi kuwekeza kwenye maabara  .

Makamu Mwenyekiti wa Mpango huo  Lucas Zakaria  amewataka Wana Rorya wote wajitokeze kuchangia ujenzi wa maabara ili kukuza elimu inayokwenda sanjari na ukuaji wa teknolojia,uchumi na maendeleo ya jamii pamoja na taifa.

Mbunge wa Rorya ,Lameck Airo amesema kuwa mpaka sasa ujenzi wa maabara umefanyika kwa asilimia 50% bado sehemu kubwa haijakamilika  hivyo wamefanya harambee hiyo lengo ikiwa ni kupata fedha za kumalizia ujenzi huo.
“Mika ijayo Rurya itakua na wataalamu wa sayansi kutokana na idadi ndogo ya maabara kama tukiamua kushikamana tutafanikisha hili la maabara” Alisema Rorya

Alisema Jumla ya Shilingi milioni 63 zilikusanywa katika harambee hiyo iliyojumuisha wenyeji wa Rory pamoja na wakazi wa Simanjiro waliojitokeza kwenye harambee hiyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top