PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: SHULE YENYE WANAFUNZI 600 YAKABILIWA NA UHABA WA MAJI NA NA MATUNDU YA CHOO JIJINI ARUSHA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Na Ferdinand Shayo,Arusha. Shule ya Msingi Engira iliyopo kata ya Themi  jijini Arusha inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa maji ...
Na Ferdinand Shayo,Arusha.


Shule ya Msingi Engira iliyopo kata ya Themi  jijini Arusha inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa maji ya kutosha licha ya kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi zaidi ya 600 hali inayoweza kukwamisha shughuli za usafi wa mazingira na afya za wanafunzi.


Mkuu wa Shule hiyo Saimon Siara amesema kuwa shule hiyo ina uhitaji mkubwa wa maji  kwa ajili ya matumizi mbali mbali na kwamba  tatizo hilo lisipotatuliwa huenda wanafunzi wakapata madhara ya kiafya.


“Tunahitaji maji kwa ajili ya kupikia,kunywa ,kuweka kwenye vyoo vya shule ili kuboresha usafi hasa watoto wanapokuwa mashuleni” Alisema Mkuu wa Shule

Ameeleza kuwa changamoto zinaikabili shule hiyo ni ukosefu wa sehemu ya kula hususani bwalo hivyo watoto hutumia madarasa na hata mazingira ya nje ambayo si salama .


Katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo Kampuni ya Bia ya TBL imetoa kiasi cha shilingi milioni 9.8 ili kusaidia ujenzi wa kisima hicho muhimu ikiwa ni moja kati ya shughuli zake za kuisaidia jamii inayowazunguka,fedha zilizotolewa na Mkuu wa kiwanda cha bia TBL kanda ya Kaskazini Salvatory Rweyemamu  na kukabidhiwa kwa Diwani wa Kata ya Themi Wallance Kinabo.

Diwani wa Kinabo amesema kuwa kampuni hiyo imekua mfano katika kuchangia maendeleo ya jamii na kuwataka waendelee kuwa wadau muhimu wa maendeleo ya jamii.

“Kwa muda mrefu shule hii imekosa kisima cha maji lakini sasa tumaini lipo tunaamini baada ya wiki mbili ujenzi wa kisima utaanza na wanafunzi watapata huduma hiyo muhimu” Alisema Kinabo



Diwani wa kata ya Themi Wallance Kinabo (CHADEMA) akionyesha choo kinachotumika katika shule ya msingi Engira kwa  Mkuu wa kiwanda cha bia TBL kanda ya Kaskazini Salvatory Rweyemamu (wakwanza kushoto) ,TBL walikabidhi kiasi cha shilingi milioni 9.8 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kisima cha Maji katika shule ya msingi Engira   .Picha na Ferdinand Shayo

  Diwani wa kata ya Themi Wallance Kinabo akipokea cheki ya shilingi milioni 9.8 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kisima cha Maji katika shule ya msingi Engira  kutoka kwa Mkuu wa kiwanda cha bia TBL kanda ya Kaskazini Salvatory Rweyemamu,katikati ni Mkuu wa shule hiyo Saimon Siara .Picha na Ferdinand Shayo

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top