PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MKURUGENZI WA TFF ATUPWA JELA MIAKA SITA, NI ELLIUD MVELLA MAARUFU KWA JINA LA MAHANJI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mvella mwenye suti ya michezo siku moja kabla hajahukumiwa MAHAKAMA ya Mkoa ya Iringa jana imemtia hatiani    Mkurugenzi wa S...

Mvella mwenye suti ya michezo siku moja kabla hajahukumiwa
MAHAKAMA ya Mkoa ya Iringa jana imemtia hatiani  Mkurugenzi wa Sheria na Utawala wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Eliud Mvella baada ya kupatikana na makosa manne ya kuendesha biashara ya bima bila kibali.

Mvella aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR Mageuzi Mkoa wa Iringa kabla ya kutimkia CCM katika miaka ya karibuni na kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) alihukumia miaka sita au kulipa faini ya Sh Milioni 3 baada ya kupatikana na hatia ya kutenda makosa hayo.

Mvella aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Iringa (IRFA) alikwepa kutumikia kifungo cha miaka sita jela baada ya kufanikiwa kulipa faini ya Sh Milioni 3 iliyolipwa kupitia risiti namba 3425607.

Mvella ambaye mjini hapa anajulikana zaidi kwa jina la Mahanji alifikishwa katika mahakama hiyo akituhumiwa kwa kosa la kwanza la kuendesha biashara ya bima bila kibali, pili kufanya shughuli za bima bila usajiri, tatu kuuza stika za bima za magari na kava noti bila kibali na nne kutoa risiti za bima bila kibali.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi Mwandamizi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa, Ruth Massam alisema Mahanji alitenda makosa hayo Mei 25, 2013 katika jengo la Higlands hall kwa kutumia kampuni ya bima hewa iliyojulikana kama Emock.

Alisema katika kosa la kwanza, mahakama hiyo imemtia hatiani Mvella na imempa adhabu ya kifungo cha miaka miwili gerezani au faini ya Sh Milioni moja.

Kwa mujibu wa hakimu huyo, Mvella amehukumiwa miaka miwili gerezani au faini ya Shmilioni moja kwa kosa la pili na kifungo cha miaka miwili au faini ya Sh Milioni moja kwa kosa la tatu na nne.

Kwa kupitia kampuni hewa ya bima ya Emock, Mvella alitenda makosa hayo kwa kutumia kampuni ya Bima ya Mwananchi yenye makao yake makuu Arusha wakati hakuwa mwajiliwa wa kampuni hiyo.

Alisema mshakiwa alikutwa na vifaa vya kampuni hiyo kwenye ofisi iliyopo jengo hilo la Highland.

Hata hivyo ofisi hiyo haikuwa na kibao cha jina la  kampuni lakini risiti zake zilikuwa zikionesha kuwa inafanya kazi za Kampuni ya Bima ya Mwananchi.

Alisema Mvella alikuwa amewaajiri wanawake wawili kwa ajili ya utoaji wa huduma hizo za bima kwa kupitia kampuni hiyo hewa ya Emock.

Wakili wa Serikali Alex Mwita aliiomba Mahakama hiyo iangalie namna ya kumpunguzia adhabu mshitakiwa huyo kwa kuwa hajawahi kutenda kosa lolote.

Hakimu alitoa fursa kwa wakili wa utetezi, Erick Nyato ambaye alimwachia mshitakiwa ajitetee mwenyewe.

Mvella alisema anaomba mahakama impunguzie adhabu kutokana na kuwa na ndugu wanaomtegemea akiwemo mama yake mzazi ambaye ana umri mkubwa na watoto wanaosoma shule na vyuo.

Alisema pia anafanya kazi za kijamii kupitia shirika la IYODEA (Iringa Youth Development Association).

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top