PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MAKALA YA SIASA: WAKATI RAISI AKITARAJIWA KUPOKEA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA MJINI DODOMA LEO BAADHI YA WAKAZI WA ARUSHA WAJA NA MTIZAMO TOFAUTI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mwanaharakati Peter Ahham anaeleza kuwa rasimu ya sita imekosa viwango vya ubora wa kisiasa   wa kimataifa ulioweka na Jumuiya za Mad...



Mwanaharakati Peter Ahham anaeleza kuwa rasimu ya sita imekosa viwango vya ubora wa kisiasa  wa kimataifa ulioweka na Jumuiya za Madola ambapo Tanzania ni mwanachama,Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Umoja wan chi za Afrika (AU) .
Viwango vya ubora wa siasa kimatiafa vinaelekeza kujali mawazo mbadala na kujali upinzani hali ni tofauti kwa Bunge la katiba.
Rasimu ya Sita imekosa uhalali kutokana na kukosekana kwa ushiriki wa chama kikuu cha upinzani pamoja na vyama vingine vya siasa.
Sio kwamba kila kitu ni kibovu katika rasimu ya sita ila kuna vipengele Muhimu vya maslahi ya taifa vimeondolewa  mfano wabunge wawe na ukomo  na wawajibishwe  .Vipengele hivyo vimeondolewa Mbunge anaweza kulala mpaka muda wake ukaisha bila kuwajibishwa.
David Mustapha ,mkazi wa Sombetini anaeleza kutokubaliana na rasimu hiyo kwa kuwa hata Mwanasheria wa Zanzibar hajakubaliana nayo yeye kama Mwakilishi anayetegemewa na Raisi wa Zanzibar na Wananchi kwa ujumla.
Mfumo wa kupiga kura kwa mitandao ya kijamii ni ubatili kwasababu ni vigumu kuamini kuwa anayepiga hiyo kura ndio mtu mwenyewe na wengine wana akaunti zaidi ya moja hiyo wanaweza kuharibu mchakato a kupiga kura.
Mkazi wa Ngaramtoni Joel Ndumbalo anaeleza kuwa maoni ya wananchi yamechakachuliwa  kwa kiasi kikubwa  na pia upande wa pili wa wapinzani haujasikilizwa  mapokezi yah ii rasimu yatakua tofauti.
Mwambanga Msigwa ,mkazi wa Sombetini  anasema kuwa  Bunge la katiba limeenda vizuri  kuna vifungu ambavyo si vizuri  mfano kipengele cha Raisi wa Zanzibar  kuwa Makamu wa Kwanza wa Raisi ,kuna hatari ya kuwa na Raisi ambaye hatujamchagua kwasababu sisi hatumchagui Raisi wa Zanzibar inapotokea dharura anashika madaraka kama Raisi kwa muda


Mwenyeji wa Unguja ambaye ni Mkazi wa Arusha Omar Bashir anaeleza kutoikubali rasimu kwa kuwa imeondoa  maoni ya wananchi juu ya kuwepo kwa serikali tatu kama ilivyopendekezwa na wananchi pia kuifanya Zanzibar iwe na heshima kama  nchi.
.
Ticter Abubakar anaeleza kuwa hata kabla ya kuangalia rasimu yenyewe mwenendo wa Bunge la katiba ulikua hauridhishi malumbano na mada ziilizokua zikijadiliwa hazimlengi Mtanzania bali zilijikia zaidi kwenye ustawi wa viongozi na maslahi yao .



MKazi wa Morombo ,Joseph Shenga afafanua kuwa kutokana na mwenendo wa Bunge hilo matarajio ya wananchi kupata katiba bora yako chini baada ya kuona rasimu ya warioba imepuuzwa kwa kiasi kikubwa.

Abdala Omari ,Rasimu imepitishwa kibabe na kwa kulazimisha  wamepindisha maoni ya wananchi yaliyopelewa na warioba rasimu tunayokubaliana nayo ni ya warioba.











 

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                              

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top