PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WENGER APEWA MKATABA MNONO NA FUNGU LA MAANA LA KUFANYA USAJILI WA KUFURU ARSENAL
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
KLABU ya Arsenal itampa Arsene Wenger Mkataba mono wa Pauni Milioni 24 na day la pauni Milioni 100 kwa ajili ya kufanya ...

KLABU ya Arsenal itampa Arsene Wenger Mkataba mono wa Pauni Milioni 24 na day la pauni Milioni 100 kwa ajili ya kufanya usajili ndani ya saa 72 zijazo, baada ya kumaliza ukame wa mataji wa miaka tisa.
  Wenger atasaini Mkataba mpya wa miaka mitatu ambao kila mwaka atalipa mshahara wa Pauni Milioni 8.
Na atapewa bajeti kubwa kihistoria kwa ajili ya kuingia sokoni kufanyia usajili, ili aiwezeshe Arsenal kutwaa taji la kwanza la ubingwa wa Ligi Kuu ya England kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2004.

Hatimaye: Arsene Wenger akiwa ameshika kwa madaha Kombe la FA, aliloshinda baada ya kuifunga Hull City 3-2 ndani ya dakika 120 Uwanja wa Wembley

Wenger ameshawishika kuongeza Mkataba baada ya kuiwezesha timu yak kuifunga Hull City Jumamosi katika fainali ya Kombe la FA - hiyo ikiwa ni mara ya tank anainua taji hilo akiwa kocha wa Arsenal na sasa atabaki Emirates.
Alipoulizwa kama Mkataba mpya utasainiwa mapema, alisema: "Ndiyo - kwa sababu ninakwenda Brazil Juni 10,".
Wenger atapewa Pauni Milioni 100 za kutumia katika dirisha la usajili na kipaumbele chake ni kuwashawishi beki wa pembeni, Bacary Sagna na keeper Lukasz Fabianski wabaki katika klabu hiyo, lakini mocha huyo wa pia pia ametambulisha wachezaji watatu wa kuongeza kuboresha kikosi chake. Nataka mshambuliaji mpya, kiungo mkabaji, kiungo mchezeshaji na beki wa kulia.
Hitman: Real Madrid striker Karim Benzema (centre) remains a top target for Arsenal
Muuwaji: Mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema (katikati) anabaki kuwa chaguo kuu la for Arsenal

Wachezaji wa Bayern Munich, Mario Mandzukic na wa Real Madrid, Karim Benzema ni miongoni mea wachezaji anaowataka Wenger. 
Nyota wa Bayer Leverkusen, Lars Bender na wa Southampton, Morgan Schneiderlin ni viungo ambao wamekuwa wakifuatiliwa kwa karibu nawasaka vipaji wa Gunners, wakati Serge Aurier wa Toulouse, Calum Chambers wa Southampton na Micah Richards wa Manchester City ni mabeki wa kulia wanaotazamiwa kuziba pengo la Sagna akiondoka.
Wenger amesema: "Kwanza inabidi tumsubiri Sagna na kuona atafanya nini - pia Fabianski. Baada ya halo itabidi tuongeze wachezaji wawili au watatu kuongeza nguvu kikosini, ni hivyo kwa kweli,".
Mkataba wa Sagna unamalizika mwezi ujao na atakuwa na mazungumzo na Manchester City wiki hii juu ya Mkataba wa miaka minne, ambao atalipwa mshahara wa Pauni 100,000 kwa wiki.
Pamoja na hayo, BIN ZUBEIRY iliripoti Jumamosi kwamba Manchester United intake kuingilia kati kuipiga bao City katika kuwania saini ya beki huyo wa kulia.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top