PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MUME WA FLORA MBASHA AJIINGIZA KATIKA KASHFA NZITOOOOOOOOOO YA UBAKAJI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Flora Mbasha akiwa na mumewe Emmanuel Mbasha anayetuhumiwa kwa ubakaji. JESHI la Polisi Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam li...


Flora Mbasha akiwa na mumewe Emmanuel Mbasha anayetuhumiwa kwa ubakaji.

JESHI la Polisi Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam linamsaka kwa udi na uvumba Emmanuel Mbasha (pichani) ambaye ni mume wa mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini, Flora Mbasha kwa madai ya kumbaka shemeji yake mwenye miaka 17 ambaye ni yatima.

Taarifa za tukio hilo ziliripotiwa Jumatatu saa 12 jioni katika Kituo cha Polisi Tabata (Tabata Shule) na kufunguliwa kesi yenye Kumbukumbu Na. TBT/RB/319/2014 na ya Jalada la Uchunguzi Na.TBT/IR/1865/2014, zikimtuhumu mwanamume huyo kwamba alimbaka binti huyo mara tatu na kumsababishia maumivu makali.

Binti huyo alifika katika kituo hicho cha polisi akiwa na ndugu zake wawili ambao walilalamika kwamba kulikuwa na jitihada kubwa kutoka upande wa mtuhumiwa wa kuzima kesi hiyo.

Akizungumza na mwanahabari wetu nje ya kituo hicho, binti huyo alisema shemejiye alimbaka mara ya kwanza, Ijumaa iliyopita na Jumapili alimbaka mara mbili ndani ya gari.

Alisema mara ya kwanza alikaa kimya baada ya mtuhumiwa kumtishia kwamba angemdhuru kama angetoa taarifa ya tukio hilo alilofanyiwa wakiwa sebuleni nyumbani kwake Tabata Kimanga, lakini aliamua kutoa taarifa kwa ndugu zake baada ya kubakwa mara ya pili.

Kauli ya Florah Mbasha
Alipoulizwa juzi Jumanne, mwimbaji huyo alisema kwa sasa hawezi kuzungumzia kwa undani tuhuma zinazomkabili mumewe na kwamba alikuwa anajisikia vibaya kutokana na tukio hilo kuhusisha watu wake wa karibu.

“Of course (bila shaka), hili sio tukio zuri. Kwa sasa sina uwezo wa kuzungumza kwa sababu hili suala lipo Polisi. I am confused (nimechanganyikiwa), ukizingatia kwamba linasemekana kutokea wakati sikuwepo nyumbani, naomba tuzungumze baada ya akili kutulia,” alisema.


Vipimo vya hospitali
Siku hiyo ya Jumatatu, baada ya tukio hilo kuripotiwa, mtoto huyo alipelekwa katika Hospitali ya Amana ambako alifunguliwa faili la matibabu na kupewa namba ya usajili 667. Aliingia chumba cha matibabu namba 21 kumuona daktari kwa ajili ya vipimo zaidi.

Matokeo ya vipimo yalionyesha kuwa binti huyo alikuwa amefanya ngono kwa nguvu. Katika fomu hiyo ya uchunguzi, daktari aliandika ‘High v5gina swab’.

Baada ya vipimo, familia ilirudi katika Kituo cha Polisi kupeleka matokeo ya vipimo vya daktari, hivyo kufungua faili la kesi lililopewa namba RB TBT/RB/319/2014 na namba TBT/IR/1865/2014.

Juzi Jumanne binti huyo alikwenda tena Amana ambako alifanyiwa vipimo vilivyobaki vya VVU na mimba. Vipimo vya awali vya VVU vilionyesha kuwa hakuwa ameathirika na hakupata ujauzito.

Historia ya Mlalamikaji( binti )
Mlalamikaji ni kati ya watoto mapacha waliozaliwa jijini Mwanza na mama ambaye jina lake halikupatikana mara moja.

Mama wa mtoto huyo (kwa sasa ni marehemu pamoja na mume wake) akiwa muumini wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God (EAGT) aliamua kumtoa mtoto mmoja kwa mama mzazi wa Flora Mbasha kwa lengo la kumlea, wakati huo mtoto huyo alikuwa na miezi mitatu.

Mama wa Flora alikaa na mtoto huyo akimsomesha hadi alipofika darasa la saba ambapo alimkabidhi kwa Flora na kuishi naye hadi alipofikwa na janga hilo.

Maelezo zaidi yanasema Mbasha aliweza kufanya kitendo hicho kwa sababu mkewe (Flora) ameondoka nyumbani na kwenda kuishi hotelini kwa kile kilichodaiwa kwamba kuna ugomvi mkubwa ndani ya ndoa yao.

Taarifa zaidi zinadai kwa sasa Mbasha naye hayupo nyumbani kwake huku mlalamikaji akidaiwa kuchukuliwa na familia ya Mchungaji Josephat Gwajima...

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top