PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Shambulizi la kigaidi lawaua 6 Kenya
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  Polisi mtaani Eastlei...


Polisi wamesema kuwa milipuko miwili ilitokea wakati magaidi waliporusha mabomu katika mkahawa mdogo ulio karibu na kituo cha mabasi mtaani humo.

Walioshuhudia shambulizi walisema kuwa walisikia mlipuko wa tatu katika eneo hilo ingawa polisi hawajathibitisha hilo.
Miongoni mwa waliojeruhiwa walikuwa wanawake ambao walipata majeraha mabaya na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Kwa mujibu wa polisi wale waliouawa walikuwa wamekwama ndani ya mkahawa huo baada ya mlango kufungwa na washambulizi waliorusha mabomu hayo ndani ya mkahawa wenyewe.
Waathiriwa walikuwa wameenda kununua chakula cha jioni. Idadi kubwa ya wakimbizi wa Somali wanaishi katika mtaa wa Eastleigh.
Inaarifiwa washambuliaji walitumia maguruneti au mabomu ya kutengezwa nyumbani kufanya mashambulizi hayo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top