PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TAASISI YA FRIEDKIN CONSERVATION FUND ( FCF) YAFADHILI MRADI WA TEMBO KUFUNGWA VIFAA VYA UTAMBUZI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Dr. Edward Kohi wa kituo cha utafiti wa wanyama pori TAWIRI akiwana Dr.Robert Fyumagwa wa TAWIRI wakimfunga kifaa cha mawasiliano...



Dr. Edward Kohi wa kituo cha utafiti wa wanyama pori TAWIRI akiwana Dr.Robert Fyumagwa wa TAWIRI wakimfunga kifaa cha mawasiliano tembo katika hifadhi ya Taifa Mikumi
Mwandishi wetu,Mikumi

Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin Conservation Fund(FCF) imejitolea kufadhili mradi wa kufungwa vifaa vya kufatilia mienendo yaTembo katika eneo la Ikolojia ya Selous hadi hifadhi ya Taifa ya Mikumi mradi utakao gharimu zaidi ya sh 1bilioni.

Akizungumzia zoezi hilo.Mtafiti kiongozi wa TAWIRI, Dk.Edward Kohi alisema,mpango huo utasaidia mapambano dhidi ya  ujangili,kudhibiti Tembo kuvamia mashamba na kujua mienendo yao.

Dk Kohi alisema, mpango huo utakuwa wa miaka mitano na tayari tembo watano wamefungwa vifaa hivyo vya mawasiliano katika eneo la hifadhi ya Taifa ya Mikumi na awamu ya kwanza Tembo 13 watafungwa vifaa hivyo na katika mradi wote tembo 60 watafungwa.

"tembo ambao watafungwa collar ni viongozi wa makundi na baada ya kufungwa watakuwa wanaonekana na wahifadhi kupitia mfumo wa mawasiliano ambao umewekwa kila wanapokuwa" alisema


Akizindua mpango huo,kwa niaba ya Mkurugenzi wa Wanyamapori, wizara ya Maliasili na Utalii,Afisa wanyamapori mkuu,Silivernus Ukudo alisema mpango huo una manufaa makubwa katika uhifadhi.

Ukudo alisema, katika eneo la ikolojia ya Selous - Mikumi ndiko kuna tembo wengi zaidi nchini ambao wanaokadiriwa kufikia 15,000.


Alisema serikali inashukuru msaada uliotolewa na mashirika ya uhifadhi Friedkin Conservation Fund  na frankfurt zoological society na WWF kwa msaada waliotoa kusaidia mpango huu.

Meneja mawasiliano wa taasisi ya Friedkin Conservation Fund,Clarence Msafiri alisema, taasisi hiyo imejitolea kusaidia zoezi hilo kwani ni muhimu kwa taifa.

Alisema FCF ambayo kampuni zake kadha zimewekeza maeneo ya hifadhi nchini,inatambua kama Tembo wakilindwa Wanyamapori wengine watakuwa salama.

"Katika zoezi hili muhimu tumetoa helkopta na misaada mingine ili kuwezesha Tembo kufungwa vifaa hivi vya mawasiliano" alisema

Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya Mikumi,Godwell Ole Meng'ataki alisema zoezi la kufungwa collar za mawasiliano litasaidia kupunguza migogoro ya uvamizi katika mashamba ya vijiji 19 vinavyozunguka hifadhi ya Mikumi.

"Pia tutaweza kufatilia maeneo ya mapito ya wanyama kutoka Mikumi hadi maeneo ya Wami mbiki na hifadhi za kusini hadi nchi jirani ya Msumbuji" alisema


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top