PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TAASISI ZAPONGEZWA KUBORESHA NANE NANE 2018 SIMIYU
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya nanenane mwaka huu mkoani Simiyu Raisi ms...
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya nanenane mwaka huu mkoani Simiyu

Raisi mstaafu wa awamu ya tatu mheshimiwa Benjamini Mkapa akikabidhi cheti cha kufanikisha maonesho ya nanenane kwa Mkurugenzi wa Friedkin Conservation Fund(FCF) Abdurkadir Mohamed mara baada ya kufunga maonesho hayo tarehe 8/8/2018


 

Mwandishi wetu, Bariadi.
 
Zaidi ya Taasisi 30 ambazo zilichangia kufanikisha maonesho ya wakulima na wafugaji Nane nane kitaifa mkoani Simiyu, zimepewa zawadi na kupongezwa na kamati ya maandalizi ya maonesho hayo.

Katibu tawala mkoa wa Simiyu, Jumanne Sigini alisema maonesho ya wakulima na wafugaji, nane nane mwaka 218 yamekuwa na mapinduzi makubwa kutokana na ushiriki wa taasisi nyingi lakini pia uchangiaji wa maonesho hayo ambao ulifanywa na wadau mbali mbali.

Sagini alitaja baadhi ya taasisi ambazo zimechangia maonesho hayo kufana ni Benki ya NBC, Taasisi ya uhifadhi a Friedkin Conservation Fund,Vituo vya luninga vya TBC na Clouds,Suma JKT, NMB bank,taasisi mbali mbali za umma  ikiwepo halmashauri zote za mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na mashirika binafsi.

Wakizungumza kuhusiana na maadhimisho ya Nane nane, Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Anthon Mtaka, Mkuu wa mkoa wa Shinyaga, Zainab Telack  na Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima, walieleza maonesho ya mwaka huu, yamekuwa na mabadiliko makubwa ambayo yanalenga mapinduzi ya kilimo na ufugaji katika kuelekea Tanzania ya Viwanda.

Mtaka alisema wameridhishwa na ushiriki wa wananchi wengi lakini pia aina ya vipando, zana za kilimo na ufugaji na huduma mbali mbali, ikiwepo kuvutia watalii, zilivyooneshwa katika maonesho hayo.

"viwanja vya Nyakabindi havitakufa baada ya maonesho, tutahakikisha vinaendelea kutumika na makundi mbali mbali katika kulima kilimo cha kisasa lakini pia kutumika kama shamba darasa la kilimo na ufugaji wa kisasa"alisema

Alisema katika maonesho ya mwakani, watajipanga kuwa ya kimataifa zaidi kwa kualika taasisi nyingi za kimataifa sambamba na nchi jirani.

Baadhi ya wakurugenzi wa taasisi zilizotunukiwa vyeti maalum, ikiwepo taasisi ya Friedkin,walisema wameshiriki maonesho hayo, ili kuonesha umuhimu wake, katika kufikia lengo la Serikali ya awamu ya tano ya Tanzania ya viwanda.

Mkurugenzi wa Friedkin Conservation Fund(FCF) Abdurkadir Mohamed, alisema taasisi yao ya utalii na uhifadhi, ilishiriki ili kuonesha mahusiano ya Utalii katika Kilimo na ufugaji nchini.

"FCF mdau wa maonesho kwani tunafanyakazi katika vijiji vya wakulima na wafugaji, hivyo tunategemea malighafi kutoka kwao lakini pia tunashirikiana katika uhifadhi wamazingira ili kupata mvua lakini pia tunashirikiana katika vita dhidi ya ujangili ili wanyama wetu waendelee kuwepo"alisema.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top