PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Ndege ya Malaysia iliyopotea na watu 298 mwaka 2014 ilipigwa na Kombora
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
    Taarifa mpya ya kuifahamu leo May 25, 2018 ni kuhusu Wapelelezi wa Uholanzi waliokuwa wakichunguza ajali ya ndege ya Malaysia MH...


   
Taarifa mpya ya kuifahamu leo May 25, 2018 ni kuhusu Wapelelezi wa Uholanzi waliokuwa wakichunguza ajali ya ndege ya Malaysia MH17, wamekamilisha uchunguzi na kuonyesha kuwa ndege hiyo ilipigwa kombora na Jeshi la Urusi.
Katika shambulizi hilo la July 17 2014 kwenye anga la Ukraine watu wote 298 waliokuwa ndani ya ndege ya Boeng 777 waliuawa wakati ikivunjika vipande ikiwa safarini kutoka Amsterdam kwenda Kuala Lumpur.

Ilipigwa na kombora aina ya BUK lililofyatuliwa kutoka eneo lililodhibitiwa na waasi nchini Ukraine. Urusi inasema hakuna silaha zake zilizotumika.

Kisa hicho kilitokea wakati wa mzozo kati ya serikali na waasia wanaoungwa mkono na Urusi.

October, 2015 kamati ya Uholanzi ilisema kuwa ndege hiyo iligongwa na kombora lililotengenezwa nchini Urusi la BUK.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top