
Pichani kulia ni Rais mstaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi sambamba na waumini wengine wakiswali swala ya sikukuu ya Eid El Fitr iliyofanyika mapema leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Al Had Mussa Salum akitoa mawaidha yake wakati wa Swala ya Eid El Fitr katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,Dkt Hussein Mwinyi akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Mhe.Salum Hapi mara baada ya kuwasili katika Swala ya Eid El Fitr iliyofanyika mapema leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam,Pichani kati ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Al Had Mussa Salum .

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Mhe.Salum Hapi mara baada ya kuwasili katika Swala ya Eid El Fitr iliyofanyika mapema leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Pichani kushoto ni Mwenyekiti wa chama cha CUF,Prof Haroun Lipumba na waumini wengine wakiwasili katika viwanja vya Mnazi mmoja kwa ajili ya kushiriki swala ya Eid El Fitr jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim akiongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Al Had Mussa Salum pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Mhe.Salum Hapi kushiriki kwenye swala ya sikukuu ya
Eid El Fitr iliyofanyika mapema leo katika viwanja vya Mnazi Mmoja,jijini Dar es Salaam.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.