PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: CHADEMA KWAZIDI KUFUKUTA DIWANI WAKE MAARUFU JIJINI ARUSHA AJIUZULU NA KUHAMIA CCM
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Diwani wa kata ya Murieti jijini Arusha Kredo Kifukwe alipokuwa akitangaza kuachia ngazi ya udiwani na kujiondoa rasmi chadema mbele ya wa...
Diwani wa kata ya Murieti jijini Arusha Kredo Kifukwe alipokuwa akitangaza kuachia ngazi ya udiwani na kujiondoa rasmi chadema mbele ya wanahabari mapema leo

 
Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Diwani wa kata ya Murriet kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kredo  Kifukwe ametangaza kujiuzulu rasmi katika Nafasi ya Udiwani wa kata hiyo iliyoko Wilaya ya Arusha mkoani Arusha .

Kredo ameeleza kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo ili aweze kutumikia jamii kama raia mwema bila kuegemea upande wowote kisiasa  lakini pia amesema kuwa juhudi zinazofanywa na Raisi John Pombe Magufuli zimemfanya ajiuzulu kwani haoni sababu ya kuendelea kumpinga kutokana na kazi nzuri anayoifanya ya kulitumikia taifa bila kujali itikadi za kisiasa.

Diwani huyo aliyejiuzulu amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kujiunga na chama chochote cha siasa kwani ataendelea kuwa raia mwema na kuitumikia jamii yake pamoja na taifa huku akiendelea kuunga mkono juhudi za Rais.

Kaimu Mkurugenzi wa jiji la Arusha Injinia Gaston Pascal amethibitisha kupokea taarifa za kujiuzulu kwa diwani huyo ambaye aliwasilisha barua ya kujiuzulu katika Ofisi za Mkurugenzi kwa mujibu wa sheria hivyo watafikisha taarifa kwa tume ya uchaguzi ili uchaguzi uweze kufanyika kuziba pengo hilo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top