Diwani wa kata ya Murieti jijini Arusha Kredo Kifukwe alipokuwa akitangaza kuachia ngazi ya udiwani na kujiondoa rasmi chadema mbele ya wanahabari mapema leo |
Home
»
yanayojiri ARUSHA
» CHADEMA KWAZIDI KUFUKUTA DIWANI WAKE MAARUFU JIJINI ARUSHA AJIUZULU NA KUHAMIA CCM
Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Diwani wa
kata ya Murriet kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Kredo Kifukwe ametangaza kujiuzulu rasmi
katika Nafasi ya Udiwani wa kata hiyo iliyoko Wilaya ya Arusha mkoani Arusha .
Kredo
ameeleza kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo ili aweze kutumikia jamii kama raia
mwema bila kuegemea upande wowote kisiasa
lakini pia amesema kuwa juhudi zinazofanywa na Raisi John Pombe Magufuli
zimemfanya ajiuzulu kwani haoni sababu ya kuendelea kumpinga kutokana na kazi
nzuri anayoifanya ya kulitumikia taifa bila kujali itikadi za kisiasa.
Diwani huyo
aliyejiuzulu amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kujiunga na chama chochote
cha siasa kwani ataendelea kuwa raia mwema na kuitumikia jamii yake pamoja na
taifa huku akiendelea kuunga mkono juhudi za Rais.
Kaimu
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Injinia Gaston Pascal amethibitisha kupokea
taarifa za kujiuzulu kwa diwani huyo ambaye aliwasilisha barua ya kujiuzulu
katika Ofisi za Mkurugenzi kwa mujibu wa sheria hivyo watafikisha taarifa kwa
tume ya uchaguzi ili uchaguzi uweze kufanyika kuziba pengo hilo.
About Author

Advertisement

Related Posts
- FRIEDKIN CONSERVATION FUND WATOA MILLIONI 84 KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO KWA JAMII YA MOYOWOSI, UVINZA NA UGALA02 Oct 20180
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya na...Read more »
- MOBISOL YASHIRIKI SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA DUNIANI, WAHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI JUA KUTUNZA MAZINGIRA17 Sep 20180
Baadhi ya wafanyakazi wa Mobisol Wakifanya usafi wa mazingira jijini Arusha mapema leo Baadhi ...Read more »
- JERRY MURRO ATOA MKWARA MZITO KWA WANAARUMERU MARA BAADA YA KUAPISHWA31 Jul 20180
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana J...Read more »
- WAANDISHI WAWASILI KWA MGANGA WA JADI ILI KUMUELIMISHA JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI KWA WATOTO WA KIKE.01 Jun 20180
Waandishi wa redio jamii tano Tanzania toka katika mikoa minne ya Arusha,Manyara,Dodoma na ...Read more »
- WAMAASAI, WASONJO WATAKIWA KUACHA UKEKETAJI01 Jun 20180
Jamii za Kimaasai na Sonjo zinazopatikana katika wilaya ya Ng...Read more »
- WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA31 May 20180
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi &nbs...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.