PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: John Mnyika aponda majibu ya Serikali kuhusu Mradi wa Maji Ruvu Juu
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mbunge wa Kibamba, John Mnyika jana alibeza majibu ya Serikali kuhusu maji yanayotoka katika Bomba la Ruvu...


Mbunge wa Kibamba, John Mnyika jana alibeza majibu ya Serikali kuhusu maji yanayotoka katika Bomba la Ruvu Juu, akisema mradi huo haujaanza kufanya kazi badala yake Serikali inatoa majibu yasiyo na uhalisia.
 
Katika swali la nyongeza, mbunge huyo alisema majibu ya Serikali kuhusu mradi huo kuwa umeanza kusambaza maji katika maeneo ya Mlandizi na vitongoji vyake; Visiga, Misugusugu, Soga, Korogwe, Picha ya Ndege, Kwa Mathias na maeneo mengine hayana ukweli.
 
Katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Mary Deo Muro alitaka kujua ni lini Serikali itawasambazia maji wananchi waishio pembezoni mwa Bomba la Ruvu Juu, Mlandizi hadi Dar es Salaam hasa maeneo ya Pangani, Lumumbana, Kidumu na Zogowale.
 
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isack Kamwelwe alisema kwa sasa maeneo mengi yameanza kupata maji ya kutosha ndani ya kilomita 12 pembezoni mwa Bomba Kuu la Ruvu Juu na kwamba, baadhi ya maeneo ambayo hayajaanza kupata maji, huduma hiyo itapatikana baada ya miradi mipya.
 
“Kwa kuanzia, mkandarasi M/S Jain Irrigation System Limited ameanza kazi ya ujenzi wa mabomba ya usambazaji maeneo ya Malamba Mawili, Msigani, Mbezi Luis, Msakuzi, Kibamba, Kiluvya, Mlonganzila na Maili Moja na atakamilisha kazi hiyo mwaka huu,” alisema Kamwelwe.
 
Alisema Serikali itaendelea kutenga fedha za usambazaji maji katika bajeti ya 2017/18, ili maeneo yote ya pembezoni mwa Bomba Kuu la Ruvu Juu toka Mlandizi hadi Dar es Salaam umbali wa kilomita 12 yapate huduma ya maji

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top