PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Mambo Manne Yanayowagusa Watanzania Kwenye Hotuba ya Trump Aliyoitoa Usiku wa Kuamkia Leo Huko Marekani..!!!
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Raisi wa marekani katika hotuba yake aliyoitoa kuamkia leo kwa saa zetu akihutubia baraza la Congress kuna mambo nimeona yanawagusa ...
Raisi wa marekani katika hotuba yake aliyoitoa kuamkia leo kwa saa zetu akihutubia baraza la Congress kuna mambo nimeona yanawagusa watanzania mambo makubwa ni yafuatayo
1.Amesema BUY AMERICAN,HIRE AMERICAN akimaanisha kuwa ajira ni kwa wamarekani na bidhaa watu wanunue za kimarekani au za makampuni ya wamarekani wawe ndani ya marekani au nje ya wamarekani.Hii ina maana kuwa kutakuwa na nafasi finyu mno kwa watanzania kuajiriwa marekani katika utawala wa TRump kwani msisitizo wake utakuwa ni kuajiri wamarekani na nafasi ya kampuni zisizokuwa za kimarekani kuuza bidhaa zao marekani zitakuwa nafasi hizo finyu sana.
2.Kuhusu Biashara ya marekani na nchi zingine.Kasema Kampuni za marekani zikiuza bidhaa nje ya nchi huwa wanachajiwa kodi kubwa sana kwa bidhaa zao sehemu zingine hadi asilimia 100 hutozwa kodi kwa bidhaa zao wakati bidhaa zinazotoka nchi hizo kuingia marekani hutozwa kodi kidogo au hazitozwi kabisa.Amesema hilo hataliruhusu tena atahakikisha na wao wakiingiza bidhaa zao marekani anawakomesha kwenye kodi.Hii ina maana gani ni kuwa kama kuingiza gari la kimarekani Tanzania huwa tunatoza ushuru wa asilimia mia moja tujiandae bidhaa zetu kuraruliwa kodi kwa kiwango hicho hicho zikiingia marekani na kutazifanya bidhaa zetu zisiweze kupenya na kushindana sokoni marekani
3.Amesema atatahakikisha inakuwa rahisi kampuni za marekani kufanya biashara ndani ya marekani na atahakikisha inakuwa vigumu kwa kampuni za marekani kutoka nje ya marekani kuhamisha mitaji na shughuli zao .Maana yake ni kuwa ata encorage uwekezaji wa ndani na ku-discourage uwekezaji nje ya marekani kwa kampuni za kimarekani.Hili lina maana kuwa kutakuwa na upungufu wa wawekezaji wa kimarekani watakaokuja kuwekeza Tanzania
4.Kuhusu UHamiaji amesema anataka wahamiaji wenye uwezo wao wa kipesa wenye pesa zao sio wale wanaotarajiwa kupata pesa za wamarekani.Anataka wenye uwezo tu wa kifedha ndio wapewe kipaumbele .Maana yake ni kuwa watanzania waenda kusaka fursa kule hawana nafasi tena Marekani anataka kutumia utaratibu wa MERIT BASED kama unaotumika canada,austarlia na newzeland

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top