PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TAMASHA LA AMANI NA UTALII KUFANYIKA JANUARY 29 JIJINI ARUSHA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Katibu wa Kamati ya Olympic Taifa.Filbert Bayi akimkabidhi zawadi mwanariadha Fabian Joseph kwa kushika nafasi ya pili michuano ya Arusha...
Katibu wa Kamati ya Olympic Taifa.Filbert Bayi akimkabidhi zawadi mwanariadha Fabian Joseph kwa kushika nafasi ya pili michuano ya Arusha tourism Marathon.zawadi ya 250,000

 


Afisa Michezo Mkoa wa Arusha.Mwanmvita Okeng'o akimkabidhi zawadi ya kwanza Angelina Tsere baada ya kushinda Arusha tourism Marathon alizawadiwa sh 500,000.




Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole   katikati akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari awapo pichani

 mkurugenzi wa kampuni ya  Arusha Media  ambaye ni mmojawapo wa waandaaji wa tamasha hili Musa Juma katikati akiwa anaongea na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo
 Akizungumzia tamasha hilo na kutaja michezo itakayokuwepo  , Mkurugenzi wa  Alfredo Shahanga  Sports Promotion ,Alfredo Shahanga katika kati
 baadhi ya waandishi wa habari wakifatilia mkutano huo





Arusha, Tamasha la Utalii mkoani Arusha,linatarajiwa kufanyika Januari 28 na 29 kwa kuwashirikisha wanahabari, wanafunzi wa vyuo na wadau wa utalii  mkoa wa Arusha.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole alisema, tamasha hilo, ambalo hufanyika kila mwaka, limeandaliwa na taasisi ya Arusha Media kwa kushirikiana na Alfredo Shahanga Sports promotion..


Alisema awali tamasha hilo, lilipangwa kufanyika Desemba 27 mwaka 2016  lakini lilisogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa  taratibu za maandalizi.

Ngobole alisema lengo la tamasha hilo ni kuhamasisha utalii wa ndani na kupinga matukio ya ujangili.


Alisema katika tamasha hilo, kutakuwa na kongamano la wanahabari kujadili mchango wa vyombo vya habari katika kukuza utalii na kupiga vita ujangili  pia sheria mpya ya vyombo vya habari.


“pia tunatarajia kuwa na maonesho ya bidhaa za utalii ili kuonesha utajiri wa maliasili zilizopo hapa nchini”alisema.


Mkurugenzi wa taasisi la Alfredo  Shahanga promotion, alisema licha ya makongamano ya masuala ya utalii, pia kutakuwa na burudani na michezo januari 29.

Alisema kutakuwa na mashindano ya riadha ya Tourism Marathon  pia michezo za soka, kuvuta kamba na ngoma mbali mbali za asili lengo ni kutangaza utalii wa Tanzania.

“hivi karibuni tutatangaza ratiba ya mashindano yote, zawadi na wadhamini”alisema.


Hizi ni baadhi ya picha katika tamasha la amani na utalii lililofanyika mwaka 2015 katika viwanja vya general tyre

Mwenyekiti wa kamati ya amani mkoa wa Arusha(APET) Petro Ahham akimkabidhi kikombe cha ushindi  wa bonanza la amani na utalii mkoa wa Arusha,nahodha wa timu ya Kitambi Noma, James Lugangira lililofanyika vuwanja vya general tyre jijini arusha
Wanamichezo wa kitambinoma wakiwa wanashabikia ushindi mara baada ya kukabidhiwa kombe katika kiwanja cha General Tyre jijini Arusha


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top