PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WAENDESHA BODABODA SAME WATAKIWA KUTII SHERIA ILI KUPUNGUZA AJALI ZA BARABARANI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule,akizungumza na waendesha bodaboda Katika ukumbi wa Halmashauri hiyo,kutoka kulia mwisho ...
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule,akizungumza na waendesha bodaboda Katika ukumbi wa Halmashauri hiyo,kutoka kulia mwisho ni,Katibu wa bodaboda Mkoa wa Kilimanjaro,Rashidi Omary,anayefuata Kateri Genesi,Katibu Hamasa  wa bodaboda Wilaya ya Same,pamoja na Charles Mchome Makamu Mwenyekiti wa bodaboda wilaya ya Same na Mkoa wa Kilimanjaro
NA: SIMON MJEMA, SAME
Rai imetolewa kwa Waendesha bodaboda Mkoani Kilimanjaro kutii sheria bila shuruti kwa kujitambua na kujithamini,kwa lengo la kuokoa vifo visivyo vya lazima,hali itakayopunguza vifo vya akina Mama Wajane na Watoto Yatima wanaotokana na Bodaboda kutokutii sheria.

Rai hiyo imetolewa na Katibu wa Bodaboda Mkoa wa Kilimanjaro,Rashidi Omary,wakati akihojiwa na Waandishi wa Habari,katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same kwenye Mkutano wa Mkuu wa Wilaya hiyo,Rosemary Staki Senyamule na waendesha bodaboda Same;Ambapo Katibu huyo ameliomba Jeshi la Polisi kusimamia sheria kwa kuwachukulia hatua wale wote wanaovunja sheria za usalama barabarani.

Mkuu wa Wilaya ya Same,Rosemary Staki Senyamule,amesema bodaboda ni ajira hivyo inawapasa kutii sheria za Usalama barabarani  kwa kuhakikisha wanavaa kofia ngumu,kutokubeba mshikaki na taratibu zingine za sheria za barabarani.Ambapo pia amewataka kutumia fursa za mikopo zinazopatikana Serikalini na kwenye Taasisi za Kifedha kama Benki.

Petro Gichinja ni mwendesha bodaboda Mjini Same,ameliomba Jeshi la Polisi kusimamia haki katika utekelezaji wa majukumu yake ili kuepukana na Tabia ya baadhi ya Watumishi wa Serikali kuendesha pikipiki bila kufuata sheria kama vile kutokuvaa Helmenti,huku boda boda wao wakikamatwa pindi wanapovunja sheria hizo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top