PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AWATAKA WANA SAME KUTOJIHUSISHA NA MADAWA YA KULEVYA!!!!!
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa,George Jackson Mbijima,akifungua na kukagua ghala la kuhifadhia mazao ya nafaka na mashine ya kusaga n...
Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa,George Jackson Mbijima,akifungua na kukagua ghala la kuhifadhia mazao ya nafaka na mashine ya kusaga na kukoboa nafaka Kijiji cha Ishinde wilayani Same,jumla ya miradi saba imezinduliwa wilayani humo.Mwenge wa uhuru umehitimisha mbio zake mkoani Kilimanjaro na kukabidhiwa Mkoani Manyara.picha na Simon Msafiri.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,George Jackson Mbijima,akikagua mitambo ya mradi wa maji uliozinduliwa na mwenge wa uhuru katika kijiji cha Ishinde siku ya jumamosi wakati mwenge ukiwa Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro kabla ya kuelekea mkoani Manyara,ambapo jumla ya miradi saba ya kiamendeleo ilizinduliwa wilayani same.Picha na Simon Msafiri.


Wakazi wa Kijiji cha Ishinde wakiwa wamebeba ndoo za maji baada ya kutwishwa na Kiongozi wa mbio za mwengeKitaifa,George Jackson Mbijima,  mara baada ya kuzindua mradi wa maji kijijini hapo,siku ya jumamosi wakati mwenge ukianza mbio zake wilaya ya Same kabla ya kumali9za na kuelekea mkoani manyara.

 NA: SIMON MJEMA, Same.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  Kitaifa,George Jackson Mbijimi,amewataka vijana na Wananchi nchini kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya kwa kuwa yamekuwa na athari kubwa katika maendeleo ya Taifa kwa kuharibu nguvu kazi ya Taifa pamoja na kusababisha maambukizi mapya ya ukimwi.

Akizungumza na Wananchi wa Wilaya ya Same katika Kata ya Hedaru,  eneo la mkesha wa mbio za mwenge,alisema Wananchi wa Wilaya ya Same wamejijengea sifa mbaya ndani na nje ya nchi kwa kilimo cha madawa ya kulevya aina ya mirungi,na kuwataka vijana na wananchi  hao,kuachana na kilimo hicho pamoja na matumizi ya mirungi kwa kuwa yanaathiri afya zao.

Mbijima amesema,maendeleo ya uchumi wa kati,ambayo  Taifa linataka kuyafikia mwaka 2025,hayataweza kufikiwa endapo changamoto ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikilikabili Taifa la Tanzania zitaendelea kupewa nafasi ya kutawala katika Jamii;Ambapo miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na Matumizi ya madawa ya kulevya na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said  Meck  Sadick,akiwasalimu wananchi katika eneo la mkesha wa Mwenge,amewaambia wananchi wa Same  waache kilimo cha mirungi kwa kuwa kinaharibu Afya,akili na kudhoofisha nguvu kazi,huku akiagiza viongozi wote wilayani  Same kuwahimiza wananchi kutunza na kununua chakula kabla bei hazijapanda ili kuepukana na njaa.

Akisoma risala ya Utii ya Wananchi wa Same,Mkuu wa Wilaya ya Same,Rosemary Stak Senyamule, amesema wameendelea kupambana na matumizi ya madawa ya kulevya kwa kuchukua hatua mbalimbali,ikiwemo kufyeka na kung`oa mimea ya mirungi,kwa kufanya misako endelevu ya wakulima,wauzaji na watumiaji wa mirungi,ambapo jumla ya ekari kumi za mirungiziliteketezwa.

Mwenge wa Uhuru umezindua jumla ya miradi saba ya kimaendeleo wilayani same Mkoani Kilimanjaro jumamosi iliyopita na kuweka jiwe la msingi,ikiwemo kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo kata ya Mabilioni kabla Mwenge wa uhuru kukabidhiwa Mkoani Manyara.Kauli mbiu ya mwenge mwaka huu ni VIJANA NI NGUVU KAZI YA TAIFA,WASHIRIKISHWE NA KUWEZESHWA.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top