PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: AFC YAIBANA TIMU YA MADINI LIGI DARAJA LA PILI.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA, YOHANA CHALLE. ARUSHA. Timu ya AFC imefanikiwa kupata pointi kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa ligi daraja la Pili (SDL) ili...

NA, YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

Timu ya AFC imefanikiwa kupata pointi kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa ligi daraja la Pili (SDL) iliyomaliza mzunguko wa kwanza, Katika mchezo uliochezwa mwishoni mwa Wiki katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

AFC waliingia uwanjani wakionekana wakiwa tofauti na michezo iliyopita huku wakikosa mabao ya wazi, kutokana na umahili wa golikipa wa Madini Sebastian Deodatus ambaye alikuwa na kazi ya ziada kuokoa michomo mingi iliyokuwa inaelekea golini mwake.
  
Hata hivyo Madini FC walifanikiwa kupata bao la kuongoza mnamo dakika ya 44 ya mchezo lililofungwa na Kelvin Kasim baada ya kupata pasi safi iliyopigwa na Nahodha wa timu hiyo Priscus Julius.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku timu ya AFC Wakiwa na lengo la kusawazisha na kuongeza bao, nao Madini Fc wakiwa na nia ya kulinda bao lao ili kujiweka katika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi hiyo.

Hata hivyo ndoto ya Timu ya Madini kuondoka na alama zote ziligonga mwamba zikiwa zimesalia dakika tatu kabla ya mchezo kumalizika baada ya Maxen Bawaziri kuisawazisha AFC kutokana na mpira wa Kona iliyochongwa na Abdala Amiri

Hata hivyo Amiri mara baada ya kufunga Bao hili alijikuta akilimwa kadi nyekundu na mwamuzi wa Mchezo huo Muhamed Chombo Kutoka Tanga kutokana na kitendo cha kushangilia huku akiwa amevua jezi ili hali tayari alikuwa na Kadi ya Njano

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top