PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: AFC KUKUTANA NA WADAU WAKE LEO.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. ARUSHA. Timu ya AFC inayojiandaa na ligi dara la pili (SDL)ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi mwishoni mwa...
NA; YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

Timu ya AFC inayojiandaa na ligi dara la pili (SDL)ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi mwishoni mwa mwezi huu, inatarajia kukutana na wadau wa timu hiyo leo (Ijumaa) katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Akizungumzia suala hilo katibu msaidizi wa timu hiyo Chazy Mwaimu, alisema kuwa lengo kuu ni kujadili maendeleo ya AFC kabla kuanza kipute cha ligi daraja la pili

“timu ya AFC ni timu ya wadau hivyo kila jambo lilnalifanyika lazima washirikishwe juu ya mwenendo wa timu yao, kwani kila mmoja ananafasi na haki akiwa kama mdau ndio maana leo tunakutana”

Mwaimu aliongeza kuwa timu hiyo imesajili wachezaji wazuri ambao watafanikisha lengo la AFC kurudi ligi kuu siku za usoni na kuwalejesha wapenzi wao waliopoteza matumaini.

AFC imeshaccheza michezo miwili ya kujipima nguvu ukiwemo mchezo dhidi ya JKT Oljoro ambao walitoshana nguvu ya kufungana bao 1-1., mchezo ambao ulikuwa maalumu kwa ajili ya mashindano ya Nyerere Cup yaliyomalizika mwishoni mwa mwezi uliopita.

Hata hivyo AFC Bado hawajaweka wazi wachezaji waliowasajili licha ya dirisha la usajili kufungwa, na hata waliotemwa pia hawajawekwa wazi, licha ya kuhaidi kuwa watakuwa na mchezo mwingine wa kujipima nguvu kabla ya dirisha la SDL Kuwa wazi.

AFC katika SDL imepangwa kundi B ikwa pamoja na ndugu zao timu yaMadini FC, Alliance FC [Mwanza] , Bulyanhulu FC [Shinyanga], JKT Rwankome [Mara], na Pamba ya Mwanza.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top