PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WATUMISHI WA SERIKALI WAMETAKIWA KUTUMIA MITANDAO KURAHISISHA UPATIKANAJI WA HUDUMA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Na Ferdinand Shayo,Arusha. Watumishi wa serikali wametakiwa kutumia mitandao hususan teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)...

Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Watumishi wa serikali wametakiwa kutumia mitandao hususan teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)  katika kuwahudumia wananchi kwa urahisi ili kuondoa adha ya upatikanaji wa huduma hizo ambazo wananchi hulazimika kuzifuata kwenye ofisi za serikali na badala yake kuhudumiwa kwa njia ya mtandao.

Njia hiyo ya mtandao inatajwa kuwa njia rahisi na ya haraka yenye ufanisi mkubwa inayopunguza suala la ucheleweshaji wa huduma muhimu za kijamii kama vile maji na umeme ambavyo vimekua vikilipiwa kwa njia ya mtandao wa simu bila kumlazimisha mtumiaji kufika ofisi zinazotoa huduma hizo.

Akizungumza katika Kongamano la siku nne 4 la  masuala ya matumizi ya  mtandao katika kuwahudumia wananchi ,Katibu Tawala mkoa wa Arusha amesema kuwa kukua kwa mtandao kumerahisisha upatikanaji wa huduma hizo hivyo Ofisi za serikali zinapaswa kutumia mitandao ili kuwafikia wananchi kwa muda mfupi na kupunguza msongamano katika ofisi za serikali

Mtendaji Mkuu wa serikali Mtandao  maarufu kama (e- government) Dr. Jabir Bakari  ametoa wito kwa mashirika ya umma kuhakikisha kuwa yanasimika na kuboresha mifumo ya TEHAMA ili iweze kuwahudumia wananchi kwa urahisi zaidi.

Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Umma ,Hab  Mkwizu amesema kuwa licha ya huduma ya mtandao kusaidia wananchi bado inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo  Kukosekana kwa usimamizi thabiti wa mfumo huo ili kuulinda dhidi ya watu wanaofanya udanganyifu kwa njia ya mtandao.

Kukua kwa teknolojia Tanzania na duniani kwa ujumla kumeifanya dunia kuwa kwenye kiganja hivyo Wananchi kupata huduma muhimu kupitia simu ya kiganjani,mapinduzi haya yakisimamiwa vizuri yanaweza kuleta tija na ufanisi mzuri kwa manufaa ya Watanzania wengi.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top