PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TEKNOLOJIA YA UMWAGILIAJI KWA NJIA YA MATONE ITAKUZA KILIMO CHA MATUNDA NA MBOGA KWA WAKULIMA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mtaalamu wa Mradi wa Kilimo chenye tija Tanzania (TAPP ), Mussa Madurufu ( anayenyosha mikono) akito...

Mtaalamu wa Mradi wa Kilimo chenye tija Tanzania (TAPP ), Mussa Madurufu ( anayenyosha mikono) akitoa elimu ya namna ya kuendesha wa kilimo cha bustani ya nyanya kwa njia ya teknolojia mpya ya umwagiliaji kwa njjia ya matone wakati wa maadhimisho ya siku ya wakulima Julai 20, 2015 katika bustani ya vipando vya mboga na matunda ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), maonesho yaliyodhaminiwa na Asasi kilele ya sekta binafsi yenye lango kuu la kuhamasisha maendeleo ya kilimo cha mazao ya horticulture Tanzania (TAHA),TAPP ,Mradi wa Tafiti Bunifu za Kilimo (iAGRI), na SUA.
Ulaji wa matunda ni muhimu kwa afya ya mwili wa binadamu.
Baadhi ya Wakulima waliokuwa wakihudhuria maonesho ya wakulima na teknolojia mpya ya umwagiliaji kwa njjia ya matone wakipita kuangalia kipando cha bamia , maonesho hayo yalifanyika julai 20, 2015 , SUA na yalidhaminiwa na Asasi kilele ya sekta binafsi yenye lango kuu la kuhamasisha maendeleo ya kilimo cha mazao ya horticulture Tanzania (TAHA),TAPP ,Mradi wa Tafiti Bunifu za Kilimo (iAGRI), na SUA.
Mtaalamu wa kilimo kutoka TAPP akiangalia ustawi wa mboga aina ya spinach.
Mtaalamu wa lishe kutoka TAHA akiwaeleza wakulima faida ya kula matunda.
Wakulima wakipatiwa mafunzo ya kilimo bora cha matunda na mbogamboga.

Na John Nditi, Morogoro

NCHI  za  Afrika Mashariki  zimeanzisha  mchakato  wa kuweka viwango  vya  ubora  wa mazao  ya kilimo cha  bustani  kinachohusisha matunda na mboga mboga  ukiwa ni mkakati wa kuwalinda walaji  na  pia kukidhi  ubora wa soko  la nchi wananchama wa Jumuiya ya nchi hizo.

Hayo yalisemwa na Makamu wa  mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Profesa  Gerald Monela , Julai 20,2015  wakati akifungua mafunzo ya maonesho  kwa wakulima ya  teknolojia  mpya kilimo cha umwagilijai  kwa njia ya matone cha bustani  ambacho huchanganywa mbolea na maji kwa wakati mmoja .

Maadhimisho yao wakulima yalidhaminiwa na Asasi kilele ya sekta binafsi yenye lango kuu la kuhamasisha maendeleo ya kilimo cha mazao ya horticulture Tanzania (TAHA), Mradi wa Kilimo chenye tija Tanzania  (TAPP) unayofadhiliwa na Shrika la Misaada la Marekani (USAID), Mradi wa Tafiti Bunifu za Kilimo (iAGRI), na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Wakulima  zaidi ya 100 wamehudhuria maonesho hayo ya teknolojia mpya ya umwagiliaji kwa njjia ya matone   ambapo walieeleza namna watakavyonufaika na tekenolojia hiyo ingawa ina  changamoto  zake .

Kwa mujibu wa Makamu wa mkuu wa SUA, sekta ya Kilimo cha bustani   ‘Hotcultural’ inakuwa kwa kiwango cha hali ya juu na waliowekeza katika kilimo hicho wameinuka kiuchumi.

 “ Teknolojia mpya ya umwagiliaji wa matone katika kilimo cha ‘horticultre’  kina faida , lakini lazima  kiwekewe viwango vya ubora ili kukidhi soko ndani na nje ya nchi” alisema Makamu wa Mkuu wa SUA.

Kwa mujbu wa Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu hicho,   kupitia kitivo cha horticulture  kimeanzisha kituo ambacho kinatumika kufundisha wakulima  na wanafunzi  kilimo hicho  kwa kufundishwa teknolojia mbalimbali  ikiwemo cha kilimo hicho.

Pamoja na hayo alitumia fursa hiyo kuiomba serikali kutengeneza mazingira mazuri kwa kushirikiana na makampuni ili kupunguza bei za viuwatilifu, pembejeo za kisasa pamoja na mbegu bora  ili kuwawezesha wakulima wadogo kumudu kuzinunua na kuleta mabadiliko  katika sekta ya kilimo.
Kwa upande wake Maneja Uhandisi Kilimo wa TAHA, Kitururu Mbwambo alisema TAHA inatoa mafunzo mbalimbali yanayolenga kunjengea mkulima uwezo wa kuzalisha mazao bora yenye viwango vinavyokubalika katika masoko.
Hata hivyo alisema , mafunzo hayo ni pamoja na mbinu bora za kilimo kwa kutumia teknolojia mbalimbali na pia yanalenga kuwajengea wadau uwezo kwenye masuala ya biashara, namna ya kuendesha vikundi ama ushirika na masuala ya fedha.

Meneja huyo wa Uhandisi Kilimo TAHA, alizitaja shughuli nyingine ni kujenga mazingira wezeshi ya biashara ya mazao ya horticulture, upatikanaji wa fedha, huduma za usafirishaji wa mazao ya aina hiyo na kugamaisha viwango vya mazao ya horticulture.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top