PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: CRDB ARUSHA WAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA KUTEMBELEA NAKUTOA MSAADA KWA KITUO CHA WATOTO YATIMA SAINT JOSEPH
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Meru jijini Arusha   Leonce Matley akikabidhi   misaada kwa Mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha St.J...
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Meru jijini Arusha  Leonce Matley akikabidhi  misaada kwa Mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha St.Joseph, Christina Mnate juzi walipotembelea kituo hicho na kutoa misaada ya chakula na vifaa vya shule katika kituo hicho kilichopo kata ya Moshono jijini Arusha ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Mtoto Afrika .Picha na Ferdinand Shayo
Mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha St.Joseph, Christina Mnate akishukuru uongozi wa CRDB tawi la Meru kwa msaada mkubwa walioutoa kwa watoto waishio katika kituo chake


Ferdinand Shayo,Arusha.


Benki ya Crdb Arusha wametembelea kituo cha watoto yatima cha
St.Joseph kilichopo kata ya moshono jijini Arusha kuelekea katika
maadhimisho ya siku ya mtoto Afrika ambapo wametoa misaada ya vyakula
na vifaa vya shule katika kituo hicho ikiwa ni njia mojawapo kuwezesha
upatikanaji wa mahitaji ya watoto yatima .


Katika kuelekea Maadhimisho ya siku ya Mtoto Afrika ambapo benki hiyo
imeadhimisha siku hiyo kwa kutembelea kituo cha watoto yatima na kutoa
zawadi pamoja na misaada ya kibinadamu.


Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Meru  Leonce Matley  iliyopo jijini
Arusha amesema kuwa ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha kuwa
anawasaidia watoto yatima na wanaoishi mazingira magumu ili waweze
kupata elimu bora itakayowakomboa kimaisha.


Mkurugenzi wa Kituo cha watoto yatima cha St.Joseph,Sister Christina
Mnate ameshukuru uongozi wa benki hiyo kwa msaada walioupata na
kuwaasa Watu binafsi wajitokeze  kuwasaidia watoto yatima na kuwapa
malezi bora badala ya kuwaachia wageni kutoka nchi za nje  ili kujenga
taifa imara.

Christina amewataka Watanzania kujenga utamaduni wa kuwasaidia watoto
yatima na wanaoishi katika mazingira magumu  badala ya kusubiria
wageni kutoka nchi za nje wafanye hivyo



Alisema kuwa Siku ya Mtoto Afrika huadhimishwa kila mwaka June 16
katika nchi zote za Afrika  bado Changamoto ya ongezeko la watoto
yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hivyo jitihada zaidi
zinahitajika kumkomboa mtoto wa kiafrika kwenye ujinga,umasikini na
maradhi.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top