PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Wapagazi (wapandisha wazungu mlimani) watakiwa kujiunga na NHIF
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Baadhi ya wapagazi wakiwa mkutano wao wa kanda mjini Arusha.ukumbi wa golden View. Mfamasia wa NHIF Mshindo Msulle akitoa mada huu...

Baadhi ya wapagazi wakiwa mkutano wao wa kanda mjini Arusha.ukumbi wa golden View.

Mfamasia wa NHIF Mshindo Msulle akitoa mada huu ya huduma za NHIF hasa maduka ya dawa ambayo wanaweza kupata madawa pindi watakapokosa hospitali.


Arusha,Zaidi ya vijana  20,000 wanaofanyakazi ya kubeba mizigo ya watalii,(wapagazi) katika Mlima Kilimanjaro na Meru ,wametakiwa kujiunga na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ili kujihakikisha huduma bora ya afya .

Meneja wa NHIF mkoa Anisia Ngweshem alitoa wito huo jana, katika mkutano wa Wapagazi , ulioandaliwa na chama cha wapagazi(TPO),uliofanyika katika ukumbi ya Golden View jijini hapa.

Ngweshem alisema, NHIF ina huduma bora za kuwapatia matibabu watanzania ikiwepo huduma mpya ya kulipia kwa mwaka 76,800 makundi maalum.

Akizungumzia huduma za afya kwa wapagazi, Mwenyekiti wa bodi ya TPO Alex Lemenge alisema chama hicho, kinaandaa utaratibu wa kuhakikisha wapagazi wote wanajiunga na mifuko ya bima za afya.

Alisema utaratibu huo, utaondoa matatizo ya wapagazi kufariki kwa kukosa huduma bora za afya kutokana na kazi ngumu wanayofanya kubeba mizigo ya watalii na kupanda milima.

Awali Makamu mwenyekiti wa TPO, Loshiye Mollel aliomba serikali kuwaunga mkono wapagazi ili waweze kupata maslahi bora ambayo ndio yatawapatia huduma bora za za afya.

“tumekuwa na mgogoro na makampuni ya utalii kwa zaidi ya mwaka sasa, tunaomba yatekeleze maelekezo ya serikali kulipa ujira kwa siku kati ya Tsh 12,000 hadi 15,000 lakini hadi sasa ni makampuni 28 tu kati ya Zaidi ya 400 ndio yanalipa”alisema.

Katika mkutano huo, wapagazi waliunga mkono, mpango wa kujiunga na NHIF  huku wakitaka uongozi wa TPO kwa kushirikiana na taasisi nyingine kushinikiza malipo bora kwa kazi yao.
mwisho


Mkutano wa chama cha  wanaofanyakazi ya kubeba mizigo  ya watalii (wapagazi ) wa mlima Kilimanjaro na Meru(TPO)  na mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF kuhamasisha wapagazi kujiunga na mifuko ya bima ya afya ili kupunguza tatizo la wapagazi kukosa huduma bora za afya.
Mkutano huu, ambao uliandamana na semina na NHIF, ulifanyika ukumbi wa Golden View jijini Arusha.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top