PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: CHADEMA ARUSHA WAZINDUA MKAKATI WA KUCHANGIWA WANANCHI NA SIMU ZA MKONONI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Katibu wa CHADEMA kanda ya Kaskazini Amani Golugwa akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya Uzinduzi wa mpango wa...
Katibu wa CHADEMA kanda ya Kaskazini Amani Golugwa akifafanua jambo
kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya Uzinduzi wa mpango wa
kuchangia Chadema kwa kutumia simu za mikononi kukiwezesha chama hicho



Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Kanda ya Kaskazini kimezindua rasmi mpango wa kuchangia chama hicho kupitia simu za mkononi ili kukiwezesha chama hicho kushinda katika Uchaguzi mkuu wa taifa utakaofanyika Octoba mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za mkoa za chama hicho ,Katibu wa Chadema kanda ya Kaskazini Amani Golugwa amesema kuwa michango itakayokusanywa na wanachama na wapenzi wa chama hicho itawawezesha  kufanya kampeni nchi nzima na kuikomboa nchi hii kwa kupata viongozi bora.

Golugwa alisema kuwa kutokana na watanzania wengi kuchoshwa na uongozi mbovu wa CCM wanahitaji kukichangia chama hicho ambacho ndicho tumaini la pekee kwa Watanzania la kuleta mabadiliko ya kweli.

“Hatutaki tushindwe kufanya kampeni kwasababu hatuna fedha hivyo tunawaomba wanachama na mashabiki wa chama hicho kukichangia chama hicho kupitia simu zao za mikononi kwa kupitia namba maalumu tutakayowapatia” Golugwa

Alisema kuwa mpango huo umeanza rasmi na unakubalika kwa mujibu wa sheria za usajili wa vyama vya siasa kuwa chama kitapata mapato yake kupitia michango mbali mbali kwa wanachama.

Katibu huyo wa Kanda ya Kaskazini Amani Golugwa amewataka polisi na vyombo vya  usalama  pamoja na tume ya uchaguzi kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa misingi ya haki na ukweli hasa katika kipindi ambacho nchi inaelekea  kwenye uchaguzi ili kuepuka kuhatarisha amani.

“Tusifanye masihara na amani ,tunahitaji tume huru na yenye uadilifu itakayofanya kazi yake vizuri bila kuegemea upande wowote” Alisema Golugwa


kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka huu.Picha na Ferdinand Shayo
    

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top