PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KUNYWA NA KUUZA POMBE SAA ZA KAZI MARUFUKU SIHA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  Na Rehema Mmbando ,Kilimanjaro Serikali wilayani siha mkoani Kilimanjaro imepiga marufuku unywaji na uuzaji wa pombe saa za kazi b...

 

Na Rehema Mmbando ,Kilimanjaro

Serikali wilayani siha mkoani Kilimanjaro imepiga marufuku unywaji na uuzaji wa pombe saa za kazi baada ya kubaini nguvu kazi ya taifa inapungua hasa kwa vijana.

Mkuu wa wilaya Siha Dr.Charles Mligwa amesema wamehamua kuchukua hatua hiyo baada ya kugundua watu wengi wanatumia muda mwingi kunywa pombe badala ya kufanya kazi.

“Tumebaini wananchi wengi hasa vijana na wanaume wengi wanatumia muda wao mwingi kunywa pombe badala ya kufanya kazi kwa manuafaa yao ndio maana kama serikali ya wilaya tumefikia hatua hiyo”Alisema Dr.Mlimwa.

Alisema pia kwa muda mrefu sasa walikuwa wakikemea tabia hiyo lakini agizo hilo lilikuwa linapuuziwa na kusema kuanzia sasa atakaye bainika kupuuzia agizo hilo kwa kuuza ama kunywa pombe saa za kazi atachukuliwa hatua za kisheria.

Hata hivyo aliwataka wananchi wa wilaya hiyo kujishughulisha na kilimo na kuzalisha chakula kwa wingi na kutaka jamii kubadilika na kufanya kazi kwa bidii,kazi zitakazowaingizia kipato.

“Masuala ya watu kulia maisha ni magumu wakati ana mikono na miguu na akili waache wafanye kazi ili wapate kipato kwa ajili yao na familia zao na kunywa pombe na kutofanya kazi sio maisha kuwa rahisi”Alimalizia Mkuu wa Wilaya Siha.

Baadhi ya wakazi wa Wilaya ya Siha wamekuwa na maoni tofauti kufuatia agizo hilo la mkuu wa Wilaya ambapo baadhi yao wamefurahishwa na agizo hilo kwa kile walichokieleza litasaidia kuokoa familia ambazo zilizoachwa kwa sababu ya ulevi,huku wengine wakisema hiyo ni nguvu ya soda tu kwani wengi wao wanategemea biashara ya uuzaji wa pombe kuendesha maisha yao na jama zao.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top