PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: LOWASA AKEMEA RUSHWA KWENYE UGAWAJI WA ARDHI NCHINI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  MBUNGE wa Monduli, Edward Lowassa, (CCM), amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali na mila wanaochukua rushw...

  Image result for LOWASSA

MBUNGE wa Monduli, Edward Lowassa, (CCM), amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali na mila wanaochukua rushwa na kuuza ardhi za wananchi wakiwemo wajane kinyume cha utaratibu.
Aidha, ameitaka jamii ya wafugaji kuelewa kuwa ardhi ni utajiri mkubwa, hivyo wailinde kwani wanavyoiuza ndiyo tatizo la ukosefu wa maeneo ya malisho ya mifugo yao linavyozidi kukua.
Lowassa, aliyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa kujadili changamoto za ardhi na mazingira wilayani Monduli uliowashirikisha wajumbe zaidi ya 400 wakiwemo viongozi wa mila (malaigwanani), viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi, (CCM) kuanzia ngazi za Vijiji, Kata na Wilaya.
Alisema kuwa tatizo la ardhi wilayani hapa ni kubwa lakini limekuwa likizidi kuongezeka kutokana na wafugaji kuuza ardhi waliyokuwa wakiitumia kwa ufugaji kwa watu wengine ambao huibadilisha matumizi na kuitumia kwa kilimo na kuendeleza makazi.
Hata hivyo, Waziri Mkuu huyo aliyejiuzulu, alisema kuwa sehemu kubwa ya ardhi ya jimbo hilo imetengwa kwa ajili ya uhifadhi wa wanyamapori na jeshi, huku eneo dogo likibaki kwa ajili ya matumizi ya wananchi ambao idadi yao imekuwa ikiongezeka, hivyo akawataka washiriki wa
mkutano huo wajadili matumizi bora na endelevu ya ardhi hiyo.

“Tumewaita hapa tujadiliane tuone tatizo liko wapi kisha tushauriane tufanye nini kulimaliza, ndiyo maana tumewaalika wataalam wa ardhi wa halmashauri na Kamaishna msaidizi wa ardhi (Kanda ya Kaskazini),
Doroth Wazala watusaidie,” alisema Lowassa.

Kwa upande wake, Mbunge wa viti maalum, Namelok Sokoine (CCM), alisema kuwa wilayani hapa kuna migogoro mingi ya ardhi kuanzia ngazi za familia
na koo, jambo linaloibua uhasama miongoni mwa jamii kutokana na wengine kuamua kupelekana mahakamani.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top