PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KINANA APOKELEWA KWA HESHIMA KUBWA KALENGA NA KUSIMIKWA UCHIEF
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye wakiwa katika mkutano wa hadhara kat...



Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye wakiwa katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Kalenga, Iringa Vijini, walipoanza ziara ya siku sita za kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 pamoja na kusikiliza kero za watu na kuzitafutia ufumbuzi.Katika mkutano huo Kinana aliitaka Serikali kuandaa utaratibu mzuri wa kuwatafutia soko la uhakika wakulima.

Kinana akivishwa vazi la kimila la wazee wa kabila la Wahehe ikiwa ni heshima kwake.

Kinana akiwa katika picha ya pamoja na wazee wa kimila baada ya kukabidhiwa mkuki.
























Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipokea kadi ya Chadema kutoka Rehema Said, wakati alipopokea wanachama wapya kutoka Chadema kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Kalenga. Wanachama wapya 21 wa Chadema walijiunga na CCM























Kinana akionyesha kadi za Chadema alizokabidhiwa wakati wa mkutano huo



Kinana akiwa amekaa na Chifu Abdul Mkwawa pamoja na wazee wa kimila wa kabila la wahehe.

Kinana akipendeza na vazi la kihehe huku akiwa na mkuki mkononi.



Kinana akihutubia katika mkutano huo huku akiwa amevalia kimila.


Kinana akihutubia huku akiwa juu ya kichuguu alichokuwa akikitumia Chifu Mkwawa enzi hizo kuwahutubia wananchi wake.



Kinana akishiriki kuvua samaki katika moja ya mabwawa ya umoja wa akina mama Kata ya Kalenga.





Kinana akishiriki kupulizia dawa katika shamba la mfano la nyanya katika Kata ya Kalenga.


Kinana akiongozana na wananchi baada ya kukagua mradi wa ufugaji samaki na shamba la nyanya katika Kata ya Kalenga

Kinana akiwa na Balozi wa Shina la CCM namba moja Kata ya Kalenga alipombelea na kuzungumza na wanachama wa CCM

Kinana akisalimiana na wananchi baada ya kuwasili katika mkutano huo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top