PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: HABARI PICHA, WATU KUMI WAMEFARIKI DUNIA NA MAJERUHI SABA KATIKA AJALI MBAYA ILIYOTOKEA MBALIZI LEO.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Hivi ndivyo ambavyo Daladala hiyo ilivyojibamiza muda mchache uliopita Eneo hili la ubavuni ndipo eneo ambalo Daladala hiyo iliingi...



Hivi ndivyo ambavyo Daladala hiyo ilivyojibamiza muda mchache uliopita

Eneo hili la ubavuni ndipo eneo ambalo Daladala hiyo iliingia na Kujigonga

Gari hilo aina ya Tata likiwa limepaki pembeni Muda mchache baada ya kupata ajali hiyo

Askari wa usalama wa Barabarani akiwa anatazama na kuchunguza zaidi ajali hiyo

Eneo ambalo Daladala hiyo iliyofumuka

Viti vikiwa vimeharibika baada ya ajali kutokea




Hivi ndivyo Daladala hiyo iliyokuwa ikitoka Mwanjelwa kuja Mbalizi ilivyo Haribika Baada ya ajali hiyo





Mashuhuda wakiwa wamelizunguka daladala hiyo kushuhudia kllichotokea

Hapa ndipo eneo ambapo ajali imetokea , Askari wa usalama wa barabarani wakiendelea kufuatilia ajali hiyo

Ilikuwa ni Ajali mbaya




Mashuhuda



Baadhi ya Majeruhi wakiwa wanatolewa katika Hospitali ya Ifisi kuelekea Hospitali ya Rufaa Mbeya


WATU kumi wakiwemo watoto wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine saba wamejeruhiwa vibaya katika ajali iliyohusisha magari mawili.




Ajali hiyo ilitokea leo majira ya saa nne asubuhi ikihusisha gari ndogo ya abiria maarufu daladala lenye namba za usajili T 237 BFB aina Toyota Hiace na gari kubwa aina ya Fuso lenye namba za usajili T 158 CSV.




Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wamesema ajali hiyo ilitokea maeneo ya Mbalizi baada ya Hiace iliyokuwa ikitokea Mbeya mjini kuelekea Mbalizi kulivaa Fuso ilikuwa ikiingia barabarani.



Walisema inasemekana dereva wa Hiace gari yake ilimshinda kutokana na kutelemka mlima mkali wa Mbalizi inagawa pia walimtupia lawama dereva wa Fuso ambaye alikuwa akiingia barabarani bila kuchukua tahadhari.



Muuguzi Mkuu wa Hospitali teule ya Ifisi Mbalizi, Sikitu Mbilinyi, ambako Majeruhi na marehemu walikimbizwa hapo alithibitisha kupokea majeruhi 7 ambapo alisema kati yao ni wanawake 3 na wanaume 4.



Alisema kati ya majeruhi hao wawili wamepewa rufaa kwenda hospitali ya Rufaa Mbeya kutokana na kuhitaji msaada zaidi huklu wengine wakiendelea kupatiwa msaada wa haraka ili kunusuru hali zao.



Mbilinyi aliongeza kuwa pia wamepokea miili ya marehemu 10 wakiwemo watoto wawili na Wanawake wanne na Wanaume wanne.



Hata hivyo majina ya majeruhi na marehemu hayajaweza kupatikana mara moja kutokana na kuwa katika hali mbaya ambapo Dereva wa Fuso akitokomea mara baada ya tukio.

NA MBEYA YETU BLOG


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top