PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Madiwani Kiteto kwenda kumwona Pinda ili awatatulie mgogoro wa ardhi
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
mwenyekiti wa HALMASHAURI YA KITETO   Ni Kuhusu kujitokeza mauaji ya wakulima na wafugaji   Wasema vigogo wapo nyuma ya migogoro hiyo NA. ...

mwenyekiti wa HALMASHAURI YA KITETO
  Ni Kuhusu kujitokeza mauaji ya wakulima na wafugaji
  Wasema vigogo wapo nyuma ya migogoro hiyo

NA. MOHAMED HAMAD     0758 222248
BARAZA la madiwani wa Halamshauri ya Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyaralimeunda tume  maalumu ya kwenda kumwona Waziri Mkuu Mizengo Pinda ilikutatua migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji  inayoendeleakurindima kila kukicha


Akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani jana (juzi) Mussa
Britoni Diwani wa (CCM) kata ya Sunya alisema kutokana na kukiukwa kwamaagizo ya Waziri Pinda juu ya kushughulikia migogoro hiyo wameamuakurejea kwake kueleza ukweli wa mambo

"Waziri Pinda aliagiza kufanyika vikao vya vijiji saba vilivyounda
hifadhi hiyo ambapo alisema anatilia shaka hifadhi hiyo akisema kamakuna hifadhi mbona alichokiona ni mashamba ya wakulima? wananchiwaulizwe kwanza kama nia yao bado ya kuendelea na hifadhi hiyo"alisemaPinda kwenye mkutano wa hadhara Wilayani humo
Pinda alisema kwa kuwa kuna utata wa mipaka uliowekwa na Halamshauri
kinyemela katika eneo hilo la Hifadhi ya Emboley Murtangos Wilayaiweke utaratibu upya na shirikishi ambao utasaidia kubainisha mipakahiyo kuondoa tatizo hilo
Kutobainishwa kwa mipaka hiyo kumeibua migogoro ya mara kwa mara wa
ardhi ambapo hadi hivi sasa kila mara maafa yanazidi kujitokeza katiya wakulima na wafugaji kwa kuingiliana kishuhuli kilimo na ufugaji

Waziri Pinda alitoa agizo hilo Jan 16 mwaka huu kutaka Halmashauri
hiyo kubainisha mipaka kazi ambayo hadi hii leo haijafanyika nakusababisha makundi hayo kutojua mipaka wako wako katika eneo ganikati ya kilimo,mifugo, makazi ama hifadhi
Wakati Serikali ikitoa agizo la kutolewa elimu kwa pande hizo Serikali
Wilayani Kiteto imeendelea kuwakamata wakulima na wafugaji nakuwafikisha kwenye vyombo vya sheria mahakamani kasha kufungwa kifungocha mwaka mmoja jela  ambapo zaidi ya watu 50 walifungwa huku 12wakiachiwa huru baada ya kukutwa ndani ya eneo hilo

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top