PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WAANDISHI WA HABARI WAENDELEA KUNG’ARA KATIKA UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  Mtangazaji wa TBC Grace Henry Kingalame  aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Nyang’halwe mkoani Geita   NA: ANDREA NGOBOLE, PMT Jana Rai...

 

Mtangazaji wa TBC Grace Henry Kingalame aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Nyang’halwe mkoani Geita 


NA: ANDREA NGOBOLE, PMT

Jana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alitangaza uteuzi  wa wakuu wa wilaya wapya 37, kuwahamisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 48 na wengine 55 kubakia katika vituo vyao vya kazi.

Kati ya wakuu wa wilaya wapya 37 walioteuliwa, majina ya waandishi wa wa habari yemejitokeza katika wateule hao.

Miongoni mwao ni mtangazaji wa muda mrefu wa shirika la utangazaji nchini TBC, Grace Henry Kingalame aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Nyang’halwe mkoani Geita, Kasilda Jeremia Mgeni aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro na Jaffar Mohamed Haniu aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

 Jaffar Mohamed Haniu aliyeteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.


 Rais ameendelea kuwaamini Wakuu wa wilaya wenye taaluma ya habari ambao amewahamisha vituo vyao vya kazi  na kuwapeleka maeneo mapya ya kazi ambao ni pamoja na Godwin Crydon Gondwe amehamishiwa wilaya ya Bahi mkoani Dodoma akitokea wilaya ya Kinondoni mkoani Daresalaam, Fatma Almas Nyangasa aliyehamishiwa kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani akitokea wilaya ya kigamboni mkoani Daresalaam na Simon Peter Simalenga aliyehamishiwa kuwa mkuu wa wilaya ya Bariadi akitokea wilaya ya Songwe.

Aidha majina ya wakuu wa wilaya wenye taaluma ya habari ambao wameachwa katika uteuzi huu mpya ni pamoja na Jerry Muro aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida ambaye nafasi yake inachukuliwa na Thomas Cornel Apson aliyehamishiwa kutoka wilaya Siha mkoani Kilimanjaro, na Gabriel Zakaria aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Busega ambaye nafasi yake inachukuliwa na Anna Jerome Gidarya aliyehamishiwa kutoka wilaya ya Ileje.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top