Na
Benny Mwaipaja
Serikali imeeleza kuwa kiasi chote
cha dola za Marekani milioni 65 zilizokopwa na Kiwanda cha Sukari cha Kagera kutoka Benki ya CRDB kwa
udhamini wa Serikali mwaka 2004
kimewekezwa nchini na hakijapelekwa kuwekeza katika nchi ya Kidemokrasia ya
Kongo.
Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma
na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa
akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Rufiji Mhe. Mohamed Omary
Mchengerwa aliyetaka kujua sababu za Serikali kumdhamini mwekezaji wa Kiwanda hicho
kukopa kiasi hicho cha fedha ambacho kimepelekwa kuwekezwa nchini Kongo wakati Tanzania ina uhaba wa sukari.
Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji
alisema kuwa uwekezaji uliofanywa katika Kiwanda cha Kagera ni wa takribani
dola za Marekani milioni 250 hivyo haiwezekani mwekezaji kukopa dola milioni 65
na kuzipeleka Congo ili hali kiwango cha uwekezaji nchini ni kikubwa.
“Mwekezaji wa Kiwanda hicho ni wa
ndani na amejitahidi kuajiri watanzania wengi hivyo Serikali ipo katika
mchakato wa kukiwezesha kiwe cha mfano
ili kiendelee kuleta matokeo chanya kwa watanzania”, alisema Dkt.
Kijaji.
Katika swali la msingi la Mbunge
huyo, alitaka kujua kiwango cha hisa ambacho Serikali inamiliki katika kiwanda
cha Sukari cha Kagera na kiasi cha fedha kilichokopwa na kulipwa na mwekezaji huyo
kupitia udhamini huo wa Serikali.
Dkt. Kijaji alieleza kuwa Serikali kwa sasa haimiliki
hisa zozote katika kiwanda hicho na kuongeza kuwa hisa zake katika kiwanda hicho ziliuzwa mwaka
2001 baada ya kukibinafsisha kiwanda hicho
kwa Kampuni ya Kagera Saw Mills
Limited.
Aidha Dkt. Kijaji alifafanua kuwa mwekezaji
wa Kiwanda hicho alikopa kiasi cha dola za Maerekani milioni 65 kwa kutumia udhamini
wa Serikali mwaka 2004, ikiwa ni udhamini (guarantee) wa kipindi cha miaka 12.
Alisema kuwa mpaka sasa kiwanda
hicho mimerejesha zaidi ya dola za Marekani milioni 56.88, sawa na asilimia
87.5 ya mkopo wote, na kwamba marejesho
ya mkopo uliobaki wa Dola milioni 8.12
yatafikia ukomo wake mwezi Julai, 2019. About Author

Advertisement

Related Posts
- TANESCO HAITAPATA FAIDA KAMWE!!! - JONH HECHE26 May 20180
Mbunge wa Tarime Vijijini (CHADEMA) John Heche amesema Shirika la U...Read more »
- MRADI WA UMEME WA STIEGLER WATENGEWA ASILIMIA 40 YA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI25 May 20180
Serikali imeonyesha dhamira yake ya dhati ya kutekeleza mkakati wa kuonge...Read more »
- MAPORI MATANO YA AKIBA MKOANI KAGERA NA GEITA KUPANDISHWA HADHI YA KUWA HIFADHI ZA TAIFA (NATIONAL PARKS)24 May 20180
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamisi Kigwangalla akizungumza bungeni alipokuwa aki...Read more »
- MAWAZIRI WANNE, SPIKA NA WABUNGE WATIFUANA24 May 20180
BAJETI ya Wizara ya Maliasili na Utalii, imepitishwa huku kukitokea msuguano mkali ...Read more »
- SERIKALI YAHIMIZA HALMASHAURI KUBUNI MIRADI YA KIMKAKATI ILI KUJIONGEZEA MAPATO22 May 20180
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, akijibu maswali Bungeni, Jijini Dodoma ...Read more »
- WAZIRI MPINA AJA NA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI18 May 20180
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina,akiwasilisha mpango na makadirio ya mapato na matumizi ...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.