PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KAMATI YA BUNGE YA ARDHI,MALIASILI NA MAZINGIRA YATEMBELEA PORI TENGEFU LA LOLIONDO KUJIONEA CHANGAMOTO ZINAZOKABILI PORI HILO
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Afisa uhusiano wa mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro walter Mairo mwenye kofia ya kepu akimuelezea waziri wa maliasili na utalii profesa ...

Afisa uhusiano wa mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro walter Mairo mwenye kofia ya kepu akimuelezea waziri wa maliasili na utalii profesa Jumanne Maghembe juu ya mchanga unaohama yaani shifting sand katika mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro.


Waziri wa Maliasili na Utalii Professa Jumanne Maghembe akiongozana na wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira walipotembelea kujionea makumbusho ya malikale ya dokta leakey ya olduvai george

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira mhandisi Atashasta Nditiyo mwenye suti  akizungumza na Afisa uhusiano wa TANAPA Pascal Shelutete katika makumbusjho ya malikale ya alipokuwa akiishi mtafiti Dokta Leakey, Kulia kabisa ni mhifadhi mkuu wa mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro dokta Manungi.

Afisa uhusiano wa Hifahi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akiwaongoza baadhi ya  wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wajumbe kamati hiyo katika mchanga unaohama yaani shifting sand


Nikiwa mbele ya lango kuu la kuingia ndani ya hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro

Baraza la wafugaji ngorongoro wakiwa katika ukumbi wa mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro
Simba wakiwa wamejipumzisha n dani ya ngorongoro crater

Baraza la wafugaji wa Ngorongoro wakiwasilisha hoja zao mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilipotembelea wilaya ya Ngorongoro kujionea changamoto na mgogoro uliopo baina ya wafugaji na wadau wa utalii
Simba wakiwa wamajipumzisha ndani ya Ngorongoro crater 

Kamati ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Mazingira juzi imetua wilaya ya Ngorongoro na kulitembelea eneo la pori tengefu,ambalo linamgogoro kwa zaidi ya miaka 20 sasa ili kusaka suluhu.


Eneo hilo, lenye kilomita za mraba 4000,limeingia katika mgogoro baada ya wizara ya Maliasili na Utalii, kutangaza uamuzi ya kutaka kulitenga eneo la kilomita 1500 kwa ajili ya uhifadhi na eneo lililobaki kurejeshwa kwa halmashauri ya Ngorongoro.

Akizungumza na waandishi wa habari, katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo,Mhandisi Atashasta Nditiye alisema wamefika Loliondo kuliona eneo hilo na baadaye watatoa ushauri kwa serikali.

Nditiye alisema wajumbe wa kamati hiyo, wamefanikiwa kupita sehemu kubwa ya eneo hilo, ambalo linapendekezwa kugawanywa ili kutengwa eneo la kilomita 1500 kwa ajili ya uhifadhi wa ikolojia ya Serengeti.

Akitoa maelezo kwa wajumbe wa kamati hiyo, Mhifadhi mkuu wa hifadhi ya Serengeti, William Mwakilema alisema kwa manufaa ya Taifa na dunia ni muhimu kutengwa eneo la kilomita 1500 ili lihifadhiwe.

Alisema eneo hilo ambalo ni mapito ya  nyumbu  kutoka hifadhi ya Masai Mara nchini Kenya, hadi Serengeti na baadaye hifadhi ya  Ngorongoro pia ndio eneo la mazalia ya nyumbu na vyanzo vya maji,limeharibiwa sana mifugo na shughuli za kibinaadamu na lisilipohifadhiwa uhai wa Serengeti upo mashakani.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa halmashauri ya Loliondo, Methew Siloma alisema msimamo wao bado wanapinga kutengwa eneo hilo kwa kuwa ni la vijiji na wanataka kutafutwa suluhu.

Mbunge wa jimbo la Geita ,Joseph Kacheku maarufu kama Msukuma alieleza udhaifu uliopo katika kutunzwa eneo hilo lakini akataka ushirikishwaji wa jamii ili kutambua umuhimu wa eneo hilo.

Wabunge wengine Grace Kiwelu na Lucy Owenya(viti maalum mkoa Kilimanjaro) walitaka kutazamwa maslahi mapana ya taifa katika kulinda ikolojia ya Serengeti.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, alisema dhamira ya serikali ni kuhakikisha Ikolojia ya Serengeti inalindwa kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top