PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: UCHAFU WA MAZINGIRA UNAASHIRIA UCHAFU WA FIKRA ZA WATANZANIA WENGI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  Na Godrich Izack,Arusha. Leo tarehe 9/12/2015 nimeiona Tanzania kwa namna tofauti sana na nimepata wasiwasi mkubwa sana. Ni baadh...
 
Na Godrich Izack,Arusha.

Leo tarehe 9/12/2015 nimeiona Tanzania kwa namna tofauti sana na nimepata wasiwasi mkubwa sana. Ni baadhi ya vitu ambavyo binafsi nilichagua kupambana navyo katika maisha yangu binafsi na jamii yangu kwa ujumla.USAFI!.Usafi akili,mwili na roho.Namaanisha usafi kuanzia ndani mpaka nje,tena kwa mtu moja moja kwanza na baade jamii nzima.

Tangu Raisi John Pombe Magufuli aingie madarakani amefanya alivyoweza,pongezi sana kwake pamoja na waziri mkuu Mh.Mjaliwa. Nilichojifunza kwa Dr.JPM ni kwamba sababu yeye ni mchapa kazi,mtu wa kufanya vitu vitokee na mtu anayesimamia vitu anavyoamini,aligundua kwamba tatizo ni watu wake anaowaongoza,watu wavivu,wazembe,wachafu,watu wanaotaka kuambiwa fanya hivi au usifanye,watu wasiofikiria nje ya box,yaani ni watu wa hivi hivi (people like this like that). Ninachokiona hapa ni kwamba raisi bado anakazi kubwa sana kwa aina ya watu anaowaongoza. Yote hii imetokana na mifumo ya uongozi iliyopita na mifumo ya maisha mabovu ya vizazi vilivyopita,mifumo inayoendelea kutafuna kizazi cha sasa.

Nimesikitika sana kuona watu wakifanya usafi sehemu ambazo walikua wanaishi kila siku,wanafanya kazi hapo kila siku, wanalala hapo hapo, wanakaa na familia zao, lakini mpaka waambiwe wafanye usafi ndio wafanye!huo ni upumbavu na uzembe wa hali ya juu. Eti watu wasomi, tena ni watu waheshima kabisa tena wenye umri kuliko hata raisi lakini kufikiria kwamba wanapokaa nipachafu na wanatakiwa wapasafishe wameshindwa. Naona ni maajabu mengine tena funga mwaka. Cha kushangaza ni kwamba nawasikia wanafurahia kabisa nakusema eti “inawezekana”,Doh!sasa nashangaa kilichokua kinawashinda ni nini?

Nimegundua kwamba kumbe uchafu sio tu kwenye mazingira yanayotuzunguka ambayo asilimia 100% sisi wenyewe ndio wazalishaji wakubwa wa taka hizo tena kwa kutokufikiria sawasawa. Uchafu mkubwa na mwingi sana upo katika fikra za hawa watu kwa sababu kinachoonekana nje ni matokea ya kilichokua na kukomaa ndani.Watanzania wengi ni wachafu wa fikra,tena uchafu uliokithiri ambayo matokeo yake ndio uzembe, uvivu, uchafu wa mazingira, ujinga, elimu mbovu, wizi, uchoyo, rushwa, matatizo ya ajira, umaskini uliokithiri, ufisadi na kutowajibika sawasawa ambavyo vyote kwa pamoja vinapelekea kuchelewa kwa maendeleo ya Nchi hii yenye kila aina ya utajiri.

Inashangaza sana kuona watu wakifukua mitaro ambayo kila siku iko hapo hapo wanapokaa na inapitisha maji na saa nyingine yanakwama hapo mpaka watu wanaugua kipindupindu lakini eti walikua hawaoni kama panatakiwa kuzibuliwa au kufanywa namna maji yapite kwa urahisi.huu si upumbavu sasa!

Watu wa kuambiwa fanya hivi au usifanye hivi wapo wengi sana ni mzigo katika kila sekta na katika nchi nzima kwa ujumla wake, na ndio hao wajanja wajanja waotimuliwa kazi na Raisi kwa aibu kwa sababu ya uchafu wao.Wengine ni kulalamika tu hakuna ajira,wako na mavyeti tu wakilalama sasa najiuliza mbona leo watu wanafanya kazi? inamaana walishindwa kuona hizo fursa kwa sababu ya upofu na uchafu uliosheheni katika fikra zao.

Kama tu kufanya usafi wa maeneo yanayowazunguka, wanapofanyia kazi wameambiwa unafikiri ni vitu vingapi hawafanyi mpaka waambiwe?Unauhakika gani vitu walivyofanya hapo awali kabla hawajaambiwa na Raisi kama walifanya sawasawa na ilivyotakiwa?Vipi wale wakandarasi wenye tenda za usafi katika majiji na manispaa nini wanafanyaga?chemba za idara ya maji zinazofanyiwa usafi leo je? Kumbe kutokomeza malaria, kipindupindu na magonjwa mengi tu inawezekana kabisa?

Nadhani tunahitaji usafi wa fikra na akili zetu kwanza.

Godrich Izack

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top