PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: ALLY MAYAI ASEMA ARUSHA KUKOSHA TIMU LIGI KUU NI AIBUU.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. ARUSHA. Mkongwe na mchambuzi wa soka nchini Ally Tembele Mayai akiwa Mkoa wa Arusha alisema kuwa Arusha kuko...
NA; YOHANA CHALLE. ARUSHA.

Mkongwe na mchambuzi wa soka nchini Ally Tembele Mayai akiwa Mkoa wa Arusha alisema kuwa Arusha kukosa hata timu moja inayoshiriki ligi kuu ni aibu kubwa kwa wakazi na viongozi wa soka mkoani hapa

Mayai ambaye ni mjumbe wa TFF katika kamati ya soka la vijana, Alisema hayo, wakati wa uzinduzi wa michuano ya airtel Rising Stars kati ya Future Stas na Chriss FC ambapo katika mchezo huo timu hizo hazikuweza kufungana.

“wapenzi nwa soka wa Mkoa wa Arusha wanatakiwa kuwadai viongozi wa soka wa mkoani hapa juu ya maendeleo katika tasnia ya soka,kwa sababu miongoni mwa majiji yenye utajiri mkubwa hapa nchini huwezi kuacha kutaja Arusha”

“Waangalie Mkoa wa Mbeya una timu mbili Tanzania Prisons, na Mbeya City wakati Tanga unatimu tatu Mgambo, Coast Union na Africans Sports, halafu Arusha haina ntimu hata moja yaani hii ni aibu kubwa sana” alisema Mayai.

Aliongeza kuwa soka la Arusha liuawa na wanaarusha wenyewe kwa kuwa maendeleo hayahitaji mtu mmoja bali ni kushirikiana wadau wote kwa pamoja na hilo kwa Arusha linawezeka.

Akitolea mfano timu ya JKT Oljoro inayoshiriki ligi daraja la kwanza alisema kuwa hapo ndipo wanapotakiwa kuanzia ili kutoa aibuu hiyo katika mkoa huu.

“Sikutegemea hatasiku moja kuona wanaarusha wanaiacha AFC ishuke hadi oligi daraja la pili kwa ilikuwa timu bora na tishio katika eramani ya soka hapa nchini laki ajabu timu hiyo inashiriki SDL na isipofanywa mikakati thabiti ianaweza kubaki hapo hapo” alisema Mayai

AFC na Madini ACF ndio timu zitakazo peperusha bendera ya Mkoa wa Arusha katika SDL msimu huu na ndi zinazopigiwa upatu kufanya vizur kutokana na maandalizi yanayofanywa

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top