PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: LEMA ASHANGAZWA NA TUME KUAHIRISHA BVR JIJINI ARUSHA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Filbert Rweyemamu Mbunge wa Arusha Mjini,Godbless Lema amesema uandikishaji wapigakura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Vo...



Filbert Rweyemamu
Mbunge wa Arusha Mjini,Godbless Lema amesema uandikishaji wapigakura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Voters Registration(BVR)lililokua lianze jana  na kuahirishwa hadi Juni 16,mwaka huu katika Kata nne za jijini Arusha limepangwa makusudi kwa lengo la kuwachosha wananchi wasijiandike.

Lema alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake baada ya kutembelea vituo vilivyokua vitumike kuandikisha wapigakura na kuzungumza na wananchi waliokua wamejitokeza kuitikia wito wa Tume ya Uchaguzi.

“Namwomba Rais Jakaya Kikwete amwondoe Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Jaji Damian Rubuva kwasababu ameshindwa kutekeleza majukumu ipasavyo na kuliweka taifa katika hali ya mashaka,jambo hili ni hatari katika nchi nyingine kuahirishwa uandikishwaji ni jambo ambalo wananchi  wangekua mitaani kwa maandamano,”alisema Lema

Awali Katibu Tawala Msaidizi wa mkoa ambaye ndiye Mratibu wa Tume ya Uchaguzi ,Richard Kwitege aliwaambia waandishi wa habari kuwa uandikishaji wa wapigakura umeahirishwa kutokana na matatizo ya kiufundi yakiwemo kuwepo kwa ongezeko la Kata mpya Sita na baadhi ya vifaa kutokufika kwa wakati.

Alisema katika mazingira hayo zoezi la uandikishaji litafanyika Juni 16,mwaka huu baada ya kujiridhisha na vifaa kupelekwa kwenye maeneo husika huku akitaka wananchi kuwapa kipaumbele watu wenye ulemavu na wazee.

Hata hivyo,Lema alisema  Chadema kimejipanga ipasavyo kupinga kila aina ya hila ya kukwamisha wananchi wenye haki ya kujiandikisha kufanya hivyo kwa wakati wakijua jimbo la Arusha ni ngome yao hivyo wako imara kupingana na hali zote.

Lema alisema inashangaza kuona kuwa suala la ongezeko la Kata kwenye Jiji la Arusha linajulikana kwa muda mrefu na halina mantiki kwani wangeweza kuanza uandikishaji kwenye Kata ambazo hazijagawanywa badala yake wametoa sababu ambazo hazikubaliki.

“Hili ni jambo ambalo halikubaliki kabisa,kwanini waanze kuandikisha kwenye Kata zilizogawanywa kama Sombetini,Elerai na Sokon I wakati kuna Kata ambazo Tume ya Uchaguzi  ingeweza kuanza uandikishaji  zikiwemo za Daraja Mbili, Terrat na nyingine,”alisema Lema

Alishauri Tume ya Uchaguzi kutumia weredi wa kuandikisha Jimbo moja kwa wakati mmoja badala ya kuchagua Kata chache jambo ambalo litawavuruga wananchi.

Hata hivyo juzi Mkuu wa mkoa wa Arusha,Felix Ntibenda katika mkutano wake na waandishi wa habari alisema maandalizi yote yalikua yamekamilika na kuwataka wananchi wajitokeze kwa wingi kushiriki katika tukio hilo la kidemokrasia
mwisho

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top