PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: LOWASSA AWEKA NIA NA KUSEMA ANA ARI, SHAUKU NA UWEZO WA KUONGOZA WATANZANIA, AKIPEWA NAFASI YA URAISI KUIONDOA NCHI KWENYE AIBU YA KUWA OMBAOMBA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Maelfu ya watu wakimsikiliza Mbunge wa Monduli Edward Ngoyae Lowassa akihutubia leo katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid  ambapo alitanga...
Maelfu ya watu wakimsikiliza Mbunge wa Monduli Edward Ngoyae Lowassa akihutubia leo katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid  ambapo alitangaza nia ya kugombea nafasi ya Uraisi katika uchaguzi mkuu wa Octoba mwaka huu.Picha na Ferdinand Shayo


Mbunge wa Monduli Edward Lowassa akihutubia wananchi waliofika katika katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid  ambapo alitangaza nia ya kugombea nafasi ya Uraisi katika uchaguzi mkuu wa Octoba mwaka huu.Picha na Ferdinand Shayo


Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Mtia nia wa Nafasi ya Uraisi ambaye ni Mbunge wa Monduli Edward Ngoyai Lowassa amesema kuwa iwapo atapata nafasi ya kuwa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ataiondoa nchi kwenye aibu ya kuwa omba omba kwa mataifa ya nje licha ya utajiri wa rasilimali nyingi za madini,gesi na mbuga za wanyama zilizopo nchini.

Lowassa amesema hayo jana wakati anatangaza nia ya kuwania nafasi hiyo katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid vilivyoko jijini Arusha ambapo amesema kuwa Tanzania kuendelea kuwa omba omba ni sifa mbaya kutokana na wingi wa rasilimali.

Moja kati ya agenda zinazomsukuma kugombea Uraisi ni pamoja na kuhakikisha kuwa ukuaji wa uchumi unaendana na ongezeko la ajira ili kuondokana na tatizo la ajira linalowakabili vijana wengi nchini .

“ Niliwahi kusema kuwa ukosefu wa ajira ni bomu linalosubiri kulipuka hivyo inahitajika mikakati na ubunifu wa kutengeneza ajira kwa vijana wetu ,naamini naweza katika hilo” Alisema Lowassa

Ameeleza kuwa Watanzania wengi wanahitaji mabadilko na iwapo atapata nafasi hiyo atasaidia kuleta mabadiliko ambayo yanatarajiwa na wengi.

Akinukuu maneno ya Hayati Baba wa Taifa alisema kuwa Watanzania wasipopata mabadiliko ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM.

Lowassa amesema kuwa vipaumbele muhimu ni pamoja na kuwekeza kwenye afya na elimu kutamsaidia Mtanzania kuwa na ustawi mzuri utakaoleta maendeleo ya jamii na taifa.

Mbunge wa Mwibara Kangi Lugola aliyehudhuria mkutano huo amesema kuwa kwa hatma ya nchi yetu inahitaji kiongozi kama Lowassa ili aweze kuifikisha nchi mahali ambapo watanzania wengi wanatamani ifike.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka wilaya ya Pangani Juma Hamidu amesema kuwa safari ya matumaini kwa Watanzania imeanza rasmi na wana matumaini makubwa na Lowassa kuwa anaweza kuiongoza nchi na kuifikisha katika mafanikio katika Nyanja zote.


KINGUNGE URAISI NI SUALA LA WANANCHI

Mwanasiasa Mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru Amesema kuwa suala la Uraisi ni suala la Wananchi ambao ni wanaamua hatma ya Raisi wanayemtaka na si vinginevyo .



Kingunge aliyehudhuria mkutano huo amesema kuwa wananchi wana nafasi kubwa ya kusema Raisi wanayemtaka  na awe na vigezo gani.

“Raisi Kikwete alisema Raisi anayetakiwa awe anakubalika na watu ndani na nje ya chama  hata nyerere alisisitiza kuwa Kiongozi lazima awe ni mtu anayekubalika na watu” Alisema Kingunge

Amempongeza Lowassa kwa kwa kutangaza nia yake na kuanzisha safari ya kuelekea ikulu na kuongeza kuwa Raisi wa Tanzania lazima awe na uwezo wa kukabiliana na umasikini.

Viongozi waliohudhuria ni Pamoja na Balozi Juma Mwapachu,Mbunge Mathayo David,Askofu Gwajima.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top