Naibu
Waziri wa Afya Dkt. Kebwe Steven Kebwe akiongea na waandishi wa habari
eneo la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati wa
kupokea na kukabidhi vifaa vya kupima dalili za ugonjwa wa Ebola.
Wengine ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Dharura na Maafa (kulia)
na Kaimu Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Cosmas Mwaifani.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa wataalam wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Kebwe Steven Kebwe amesema kuwa kuwasili kwa vifaa hivyo ni moja ya juhudi za Serikali za kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa salama kwa kuuzuia ugonjwa huo kuingia nchini.
Moja
ya kamera kati ya nne zilizoagizwa na Serikali kupimia dalili za
ugonjwa wa Ebola maeneo ya viwanja vya ndege. Kifaa hicho kina uwezo wa
kutunza picha na kumbukumbu za msafiri, muda , joto la msafiri, tarehe
aliyoingia nchini pia uwezo wa kupata takwimu kutoka kwenye hali ya
majimaji au jasho la binadamu pindi kinapoelekezwa kwake.
na maeneo yanayotumiwa na raia wa kigeni kuingia nchini vikiwemo vya Dar es salaam, Zanzibar, Kilimanjaro,Mbeya na Mwanza.
Ameongeza kuwa Serikali inaendelea na mpango wa kuagiza vifaa zaidi vya kuwezesha shughuli ya upimaji wa afya kwa wasafiri wanaotembea (scanners) zitakazowezesha kubaini afya za wasafiri wengi zaidi kwa wakati mmoja bila kulazimu kuwasimamisha.
Aidha, amewataka wataalam hao wa afya kufanya kazi zao kwa weledi mkubwa kwa kuhakikisha wanawapima abiria wote wanaotoka nje ya nchi bila kujali hadhi walizonazo ili kuweza kubaini kama wana maabukizi au dalili za ugonjwa wa Ebola.
“Nataka mfanye kazi yenu kwa kuzingatia weledi wa taaluma yenu na kwa kuzingatia yale mliyojifunza,mvitumie vifaa hivyo kupima kila abiria ili kubaini joto lake bila kujali cheo wala hadhi yake maana janga hili ni kubwa,” amesema Dkt. Kebwe.
Post a Comment