PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: HABARI PICHA-UZINDUZI WA JIKO LEVOLOSI ILI KUWEZESHA MPANGO WA CHAKULA MASHULENI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela akiwatunza wanafunzi wa shule ya msingi Levolosi iliyoko jijini Arusha walioimba shairi katika uz...

Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela akiwatunza wanafunzi wa shule ya msingi Levolosi iliyoko jijini Arusha walioimba shairi katika uzinduzi wa jiko lilojengwa na mhisani Daniel Materi kwa gharama ya sh milioni 25 ikiwa ni jitihada ya kuunga mkono mpango wa chakula mashuleni.ulifanyika juziPicha na Ferdinand Shayo
 


Kushoto ni Mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka na Mfanyabiashara Daniel Materi akiwatunza wanafunzi wa shule ya msingi Levolosi iliyoko jijini Arusha  walioimba shairi katika uzinduzi wa jiko lilojengwa na mhisani Daniel Materi kwa gharama ya sh milioni 25 ikiwa ni jitihada ya kuunga mkono mpango wa chakula mashuleni.Picha na Ferdinand Shayo

Aliyesimama ni Mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka akifafanua jambo mbele ya wanafunzi na wadau mbalimbali katika uzinduzi wa jiko la shule ya  msingi Levolosi iliyoko jijini Arusha lililojengwa na mhisani Daniel Materi kwa gharama ya sh milioni 25 ikiwa ni jitihada ya kuunga mkono mpango wa chakula mashuleni.kushoto ni Diwani wa kata ya Levolosi Ephata Nanyaro,wapili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha John Mongela,watatu kulia ni mkuu wa shule hiyo Elisante Kaaya na wakwanza kulia ni mhisani Daniel Materi Picha na Ferdinand Shayo

Diwani wa kata ya Levolisi Ephata Nanyaro wakisemezana jambo na Mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka katika Uzinduzi wa jiko la shule ya  msingi Levolosi iliyoko jijini Arusha lilojengwa na mhisani Daniel Materi kwa gharama ya sh milioni 25 ikiwa ni jitihada ya kuunga mkono mpango wa chakula mashuleni.Picha na Ferdinand Shayo

Na Ferdinand Shayo,Arusha
Shule ya Msingi Levolosi iliyoko jijini Arusha inakabiliwa na ukosefu wa vifaa vya kufundishia na kujifunza teknolojia ya habari na  mawasiliano (TEHAMA) ikiwemo kompyuta.
Licha ya serikali kuhamasisha matumizi ya TEHAMA mashuleni ili kusaidia kutunza kumbukumbu ya vitabu vingi na kujifunza kwa njia ya kisasa hata sehemu zenye uhaba wa walimu  bado shule nyingi za msingi na zile za kata hazina kompyuta.
Aidha Mkuu wa shule ya msingi levolosi Elisante Kaaya amesema kuwa wamekua wakikosa sehemu maalumu ya wanafunzi kujipatia  huduma ya chakula (bwalo)  na kueleza kuwa changamotonyingine wanazokutana nazo ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya kufundishianakujifunzia Tehama  kama kompyuta.
Akisoma taarifa ya shule hiyo katika uzinduzi  wa jiko la shule hiyo  lilojengwa kwa msaada wa Mfanyabiashara Daniel Materi  ikiwani njiamojawapo ya kuunga mkono juhudi za kufanikisha mpango wa chakula mashuleni.
Elisante Kaaya amewapongeza wadau wote waliojitoa kuwezesha watotowa shule hiyo kupata uji kwani mwakani wanatarajia watoto watapata hudumaya chakula cha mchana shuleni hapo.
Mbunge wa Manyara Christopher Ole Sendeka amesema kuwa  ni jukumu la jamii kujitoa kusaidia watoto waweze kusoma na kuzingatia taaluma ili waweze kufaulu.
Hata hivyo mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela amesema kuwa ni juhudi nzuri zilizofanywa na ndugu Daniel  Materi  na kuwataka wafanyabiashara wengine waige mfano wake.
Daniel amesema kuwa msaada huo ni mchango wa kuisaidia jamii inayomzunguka hususani katikamasuala ya elimu ambayo ni muhimu kwa jamii yetu

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top