PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TANZANIA YAANZA UCHIMBAJI WA URANIUM
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Tanzania itatia saini na Kampuni ya Mantra ili kuanza uchimbaji wa madini ya Uranium katika eneo la Mkuju katika hifadhi ya Selous. ...


Tanzania itatia saini na Kampuni ya Mantra ili kuanza uchimbaji wa madini ya Uranium katika eneo la Mkuju katika hifadhi ya Selous.
Waziri wa Utalii na mali asili Lazaro Nyalandu, amesema makubaliano hayo yatatiwa saini kabla ya mwisho mwa mwezi juni mwaka huu.

Mkataba huo utawezesha kampuni hiyo kuanza uchimbaji wa uranium huo ukiwa ndio mradi wa kwanza wa kuchimba masini hayo nchini Tanzania na unatarajiwa kuiletea serikali dola milioni $640 kwa mwaka.

Waziri Nyalandu alisema uchimbaji huo utafanyika katika eneo la kilomita 350 mraba kwenye hifadhi hiyo ilioko kusini mwa Tanzania.

Udhibiti wa shughuli za urani

Taarifa ya serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, imeahidi kuwahakikishia Watanzania na wananchi wanaoishi karibu na maeneo yaliyogundulika kuwepo na madini ya Urani kwa kiwango cha kuchimbwa kibiashara, kwamba Serikali imechukua hatua kadhaa za kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya shughuli za utafutaji, uchimbaji na usafirishaji nje ya nchi madini ya Urani.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, katika kipindi cha muda mrefu Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini ilisema imejiandaa kutekeleza mradi wa madini ya urani(uranium) katika eneo la Mkuju Wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma, huku mradi wa mto huo uliopo ndani ya  pori la akiba la  Wanyamapori la Selous (Selous Game Reserve) ambayo ipo katika eneo la Sehemu ya Urithi wa Dunia (World Heritage Site).
Kutokana na umuhimu wa eneo hilo Mwezi Julai 2012, World Heritage Committee iliyoko chini ya shirika la UNESCO ilitoa idhini ya kuondoa eneo la Mradi wa Mto Mkuju kwenye eneo la Urithi wa Dunia ili uchimbaji uweze kufanyika ambapo pia uchambuzi wa masuala ya mazingira katika eneo la mradi wa madini ya Uranium ulikamilika mwezi Oktoba, 2012 na hati ya Mazingira (Environmental Impact Assessment Certificate) ilitolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top