Habari zinaarifu kuwa ili Diamond Platnumz aweze kumuoa Wema Sepetu ni lazima atoe shilingi milioni mil. 100.
Habari hizi ni kwa mujibu wa gazeti moja la udaku
lililotoka Jana ambapo liliripoti kuwa mama Wema sepetu anataka
mahari ya milioni 90 na ushee ili binti yake huyo asiyechuja umaarufu
awe mkwe wa mama Diamond.
Inadaiwa kuwa sherehe za birthday za Wema na Diamond zilizofanyika hivi karibuni na kugharimu pesa nyingi ndiyo zinadaiwa kumtia hamasa mama
Wema na kutaka mahari hiyo kubwa kwa madai kuwa Diamond anazo pesa na
hashindwi kutoa pesa hiyo ili kumuoa Wema ambaye umaarufu wao wote
wawili ni mkubwa sana hapa Tanzaia huku umaarufu wa Diamond nje ya
Tanzania ukiwa mkubwa zaidi kuliko wa Wema.
Hata hivyo habari zaidi zinadai kuwa Wema mwenyewe yupo tayari kuolewa hata bure na Diamond.
Post a Comment