PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Mama Wema ataka mahari ya Mil.100 ili Diamond amuoe mwanae...Lakini Wema Sepetu asema yupo tayari kuolewa hata bure na Diamond
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Habari ya mjini hivi sasa ni Ndoa ya msataa wa Bongo , Wema Sepetu na Diamond Platnumz. Habari zinaarifu kuwa ili...


Habari ya mjini hivi sasa ni Ndoa ya msataa wa Bongo, Wema Sepetu na Diamond Platnumz.
Habari zinaarifu kuwa ili Diamond Platnumz aweze kumuoa Wema Sepetu ni lazima atoe shilingi milioni mil. 100.
Habari hizi ni kwa mujibu wa gazeti moja la udaku lililotoka Jana ambapo liliripoti kuwa mama Wema sepetu anataka mahari ya milioni 90 na ushee ili binti yake huyo asiyechuja umaarufu awe mkwe wa mama Diamond.
Inadaiwa kuwa sherehe za birthday za Wema na Diamond zilizofanyika hivi karibuni na kugharimu pesa nyingi ndiyo zinadaiwa kumtia hamasa mama Wema na kutaka mahari hiyo kubwa kwa madai kuwa Diamond anazo pesa na hashindwi kutoa pesa hiyo ili kumuoa Wema ambaye umaarufu wao wote wawili ni mkubwa sana hapa Tanzaia huku umaarufu wa Diamond nje ya Tanzania ukiwa mkubwa zaidi kuliko wa Wema.

Hata hivyo habari zaidi zinadai kuwa Wema mwenyewe yupo tayari kuolewa hata bure na Diamond.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top