PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: ARUSHA AIRTEL RISING STARS YATUA DAR
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. PRINCEMEDIATZ Kikosi cha timu ya miguu ya wanawake Arusha Airtel Rising Stars walio na umri chini ya miaka 17 ki...
NA; YOHANA CHALLE. PRINCEMEDIATZ


Kikosi cha timu ya miguu ya wanawake Arusha Airtel Rising Stars walio na umri chini ya miaka 17 kimeondoka jana (leo ijumaa) jijini hapa kikiwa na wachezaji 16 kuelekea jijini Dar es salaam katika mashindano ya Kumpata bingwa wa Mkoa katika mashindano hayo.

Akizungumza na gazeti hili kocha mkuu wa timu hiyo Jophrey Mlope alisema kuwa kikosi chake kimekamilika vilivyo kwa ajili kupambana na hatimaye kuibuka washindi.

“nawahaidi wakazi wa Arusha kuwa kikosi hiki ni imara na ninauhakika wa kurudi na ushindi, vinaja bado wana hari ya ushindani na nimekuwa nao kwa zaidi ya wiki mbili wakiwa wanafanya mazoezi asubuhi na jioni” alisema Mlope

“soka la wanawake linahitaji juhudi za ziada kuanzia kata hadi taifa, japo watu wengi wanaipa kisogo soka la wanawake na Arusha hii ina vijana wengi sana ambao wangeweza kuinuka kupitia soka, hata ukiangalia uchaguzi wa viongozi wa soka kwa wanawake kuna sua sua kutokana na mwamko kuwa mdogo” aliongeza kusema Mlope

Pia alikisefu Chama cha soka Mkoa wa Arusha (ARFA) kupitia katibu mkuu Adam Brown kwa ushirikiano wao kama chama waliouonesha kwao tangu mchakato ulipoanza na hatimaye kupata timu

“kwangu niwapongeze ARFA ambao wanajitahidi sana kwenye nafasi zao kama viongozi na kama walezi, tatizo kubwa lipo kwa wadau hapa Arusha hawajitokezi kusapoti timu, kwa sababu muda wote viongozi ndio wanajitahidi kuangalia mambo yasiende kombo na kuna vitu vingine vilitakiwa vifanywe na wadau” alisema Mlope.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top